• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

RC ANDENGENYE AZINDUA MOANGO WA UREJESHI KWA WATOTO WALIO NJE YA MFUMO WA KIMASOMO

Posted on: November 11th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Thobias Andengenye leo Novemba 11,2024 amezindua rasmi Kampeni ya kuwaandikisha na kuwarejesha shuleni watoto walio nje ya Mfumo wa Shule ngazi ya ELIMU Msingi wanafunzi waliokatisha masomo mkoani Kigoma kwa sababu mbalimbali ikiwemo vikwazo vya kijamii na kifikra.

Kampeni hiyo inaratibiwa na Serikali kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia Watoto katika Mataifa yanayoendelea(UNICEF) imelenga kuondoa vikwazo ambavyo vimekuwa vikichangia watoto kushindwa kufikia malengo yao ya kitaaluma ikiwemo ukosefu wa vifaa vya shule,utoro, Imani za kishirikina, mila potofu, matumizi ya watoto kama nguvu kazi ya familia,  hofu kutokana na adhabu shuleni pamoja na migogoro ya kifamilia.

Amesema katika kipindi cha Mwaka 2023/2024 wanafunzi walioandikishwa nje ya Mfumo rasmi mkoani Kigoma ni 12517 ambapo wavulana wakiwa 6515 na wasichana 6002. Aidha watoto waliacha utoro na kurejea shule katika kipindi hicho  wakiwa 2352 ambapo wavulana ni 1103 na wasichana 1249.

Amesema kwa mujibu wa takwimu za Mwaka 2024, idadi ya watoto walio nje ya mfumo rasmi wa Elimu ni 7,475 ambapo wavulana ni 4,124 na wasichana 3,351, wakiwa na umri kati ya miaka saba hadi 15. ‘‘Lengo letu ni kuhakikisha kwa mwaka ujao wa 2025 tunaandikisha watoto 5,632na kurejesha wanafunzi 2001’’ amesema Andengenye.

Amesema Kampeni hiyo itakuwa na msukumo mkubwa katika kuhakikisha viongozi katika ngazi za vijiji, kata, ngazi za Halmashauri pamoja na kamati za shule ili kuhamasisha na kufuatilia urejeshwaji wa watoto shuleni kwa wale waliocha sambamba na kuwaandikisha shule watoto wote waliofikia umri stahili.

Amesisitiza kuwa, kupitia Kampeni hiyo, Halmashauri za  wilaya kupitia kwa wakurugenzi na viongozi mbalimbali zitasimamia ili kuhakikisha uandikishwaji na urejeshwaji wa wanafunzi mashuleni unafanyika sambamba na kudhibiti  vichochezi vya watoto kuacha shule  ikiwemo ndoa za utotoni, ajira za watoto pamoja na vizuizi vinginevyo vya kijamii.

Sambamba na hayo, mkuu huyo wa mkoa amewahimiza wakazi kushirikiana na viongozi na wasimamizi wa masuala ya kitaaluma ili kudhibiti utoro, kutoa msaada wa kisaikolojia kwa watoto   wanaosoma pale wanapokutana na changamoto za kimaisha, kuhimiza nidhamu chanya sambamba na Halmashauri kushirikiana na wadau katika  kutoa misaada kwa watoto wanaotoka kwenye kaya zenye uhitaji mkubwa kupitia mpango wa TASAF.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa