• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

RC ANDENGENYE AZINDUA KAMPENI YA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA UMEME KWA AJILI YA KUPIKIA KWA MKOA WA KIGOMA

Posted on: October 4th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Thobias Andengenye amezindua Kampeni ya Matumizi ya Nishati Safi ya Umeme kwa ajili ya kupikia kwa Mkoa wa Kigoma kupitia Programu ya Pamoja ya Kigoma(UN-Kigoma Joint Program) na kusisitiza kuwa Kampeni hiyo itapunguza changamoto za kiafya kwa wakazi na zile za kimazingira zinazoukumba mkoa wa Kigoma kutokana na matumizi ya kuni.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni  hiyo uliofanyika katika Hoteli ya Lake Tanganyika Mjini Kigoma, Mhe. Andengenye amesema upatikanaji na Matumizi ya Nishati safi unagusa nyanja mbalimbali katika maisha ya wakazi, uendelevu wa viumbe hai sambamba na utunzaji wa Mazingira kwa ujumla.

Andengenye amesema uzinduzi wa Kampeni hiyo ya kupika kwa kutumia umeme ni sehemu ya mabadiliko yanayoendana na kuunganishwa kwa mkoa katika  Umeme wa Gridi ya Taifa na kuipa fursa  jamii mkoani Kigoma kunufaika kikamilifu na upatikanaji na matumizi ya nishati safi.


Katika hatua nyingine Mhe. Andengenye amefurahishwa na uwepo wa shule za sekondari 17 mkoani humo zinazotumia nishati safi ya Mkaa mbadala kwa ajili ya kupikia na kuachana na matumizi ya kuni na Mkaa.

Upande wake Mwakilishi kutoka  TANESCO Makao Makuu, Mha.  Samwel Luckas amesema lengo la serikali ni kuhakikisha watanzania wanahamia kwenye matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Amesema mpango huo umelenga kuwawezesha wapishi kuandaa chakula salama, kisafi na kwa gharama nafuu za upishi na kuziwezesha familia kuishi maisha salama kiafya sambamba na kupata nafuu ya kiuchumi.

"TANESCO itaendelea kusogeza karibu huduma za umeme kupitia usambazaji wa huduma hiyo ili kila mwananchi aweze kushiriki kwenye mpango huo" amesema Mha. Luckas.

Naye Mwakilishi kutoka TIB Development Bank Andrew Mwampaghale amesema taasisi yao itaendelea kuhakikisha majiko ya Nishati safi yanapatikana kwa njia ya ruzuku ili kuwapa wananchi unafuu.

"TID kwa kushirikiana na UNIDO tunaendelea kutafuta ufadhili utakaotuwezesha kupata majiko ya Umeme ambayo utafiti unaonesha hayana gharama kubwa kimatumizi na ni salama ukilinganisha na matumizi ya kuni au mkaa" amefanua Mwampaghale.




Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa