• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

RC ANDENGENYE AWAONYA WASIO NA SIFA KUTOJISAJILI NIDA

Posted on: April 13th, 2023

Raia wa Kigeni pamoja wakazi wenyeji Mkoani Kigoma wametakiwa kuepuka kufanya udanganyifu ili kupata uhalali wa kupatiwa vitambulisho vya Taifa.  

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Thobias Andengenye ametoa Rai  hiyo  alipozindua zoezi la ugawaji wa Vitambulisho vya Taifa (NIDA) ambapo Jumla ya Kadi 77281 zimekamilika na kuanza kukabidhiwa kwa walengwa katika Wilaya ya Kigoma.

Amesema baadhi ya wakazi wasio na sifa pamoja na Raia wa kigeni wamekuwa kikwazo kikubwa katika kuhakikisha zoezi la ukusanyaji taarifa kwa ajili ya kuandaa vitambulisho vya Taifa linafanyika kwa wakati.

Andengenye amefafanua kuwa, kutokana na mkoa kupakana na nchi jirani, kumekuwepo na muingiliano mkubwa wa raia kutoka nchi hizo, ambapo ameahidi  Serikali mkoani Kigoma kuendelea kufanyia kazi changamoto hiyo ili wenye zifa waweze kupata vitambulisho kwa wakati.

‘‘Changamoto ya utoaji wa Kadi za Vitambulisho vya Taifa ni endelevu kutokana na ongezeko la wageni pamoja na idadi ya wenye sifa kila siku, hivyo niwasisitize kuendelea kutoa taarifa za kweli na uhakika huku tukiisaidia Serikali kuwabaini wasio na Sifa ili kurahisisha utekelezaji wa zoezi hili’’ amesisitiza.

Aidha Andengenye amemshukuru Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi nzuri anayoifanya hususani katika Mkoa wa Kigoma kwa kuendelea  kutoa Fedha nyingi kwa ajili ya kuboresha Miundombinu ya Uchukuzi, usafirishaji pamoja na kuimarisha Sekta za Elimu, Afya na Maji.

Akiwasilisha Taarifa ya utendaji kazi, Afisa Usajili Ofisi ya Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa Mkoa wa Kigoma Odoyo Godwin amesema mpaka kufikia April 12, 2023 wamefanikiwa kusajili walengwa 967,013 huku waliopata Namba ya utambulisho hadi kufikia tarehe hiyo ikiwa ni walengwa 585,536 na waliopata vitambulisho ikiwa 273,460.

Amefafanua kuwa, kwa wilaya ya Kigoma inayojumuisha Halmashauri ya Kigoma Vijijini pamoja na Manispaa ya Kigoma/Ujiji, jumla ya vitambulisho 77,281 vimekamilika na vinaendelea kugawiwa kwa walengwa.

Amezitaja changamoto zinazochangia kuzorotesha ufanisi na uharaka katika upatikanaji wa vitambulisho hivyo kuwa ni baadhi ya wananchi kujiandikisha zaidi ya mara moja, kutopatikana kwa Namba za Simu zilizotumika wakati wa usajili wa awali pamoja na uwepo wa kundi kubwa la walowezi, wakimbizi pamoja na wageni wakazi.

‘‘Nitoe Rai kwa wanchi wote wanaostahili kupata vitambulisho kuhakikisha wanatoa taarifa sahihi ili kuepuka usumbufu wa kupata kitambulisho kwa wakati pamoja na kuepuka usumbufu inapotokea taarifa zao kutofautiana pale zinapohitajika kwa ajili ya kufanikisha masuala mbalimbali ya kiserikali’’ amesisitiza Godwin.

Baadhi ya wakazi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji waliojitokeza katika hafla hiyo wameipongeza Serikali kwa kufanikisha upatikanaji wa vitambulisho hivyo, huku wakisisitiza watendaji wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa kuendelea kutoa Elimu kwa wananchi ili kupunguza dosari zinazosababisha walengwa kusubiri kupata vitambulisho hivyo kwa muda mrefu.


Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa