• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

RC ANDENGENYE AWAASA MAAFISA USHIRIKA MKOANI KIGOMA KUTOA KIPAUMBELE KWA MAKUNDI MAALUM.

Posted on: August 26th, 2022

Pikipiki nane  aina ya Boxer zilizotolewa na Wizara ya Kilimo kupitia Tume ya Maendeleo na Ushirika kwa Mkoa wa Kigoma zikiwa tayari kugawiwa kwa Maafisa Ugani wa Halmashauri za Mkoa wa Kigoma leo Tarehe 26, Agosti 2022.

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye akijiandaa kuendesha mojawapo ya Pikipiki zilizotolewa kwa maafisa Ushirika Mkoani hapa mara baada ya kuzindua zoezi la makabidhiano ya vitendea kazi hivyo. zoezi hilo limefanyika katika viunga vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma.

Maafisa Ushirika Mkoani Kigoma wametakiwa kusimamia vyama vya Ushirika kwa nguvu mpya huku wakiyapa kipaumbele makundi Maalum ya kijamii ili yaweze kujikwamua na kujiendeleza kiuchumi.

Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Kamishna Mstaafu wa Jeshi la Zimamoto na Ukoaji Thobias Andengenye, wakati wa hafla fupi ya kukabidhi  Pikipiki  nane zilizotolewa na Serikali kwa Maafisa Ushirika wa wilaya ili kuongeza ufanisi katika utendaji kazi.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema, vyama vya ushirika vijumuishe na kuzingatia makundi ya watu wenye mahitaji Maalum, Bodaboda, Wanawake, wazee, mamalishe na makundi mengine yanayohitaji kupewa kipaumbele ili nao waweze kunufaika na Rasilimali za Serikali.

Amesema pamoja na watendaji hao wa Serikali kuhudumia Jamii kwa ujumla, wanatakiwa kuyatazama makundi hayo, kuyashirikisha na kuyawezesha kikamilifu ili kunufaika na fursa mbalimbali za kiuchumi zinazotolewa na kusimamiwa na Serikali.

Aidha, amewaasa kutumia vitendea kazi hivyo kwa kuzingatia malengo yaliyokusudiwa na Serikali, na kuepuka matumizi ambayo ni kinyume na malengo jambo ambalo ni  ukiukwaji wa maadili ya Utumishi wa Umma.

Pia,  ametoa Rai kwa Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali  za Mitaa kusimamia matumizi bora ya vitendea kazi hivyo pamoja na  kuwezesha mafuta na ukarabati ili watendaji wasikwame katika utekelezaji wa majukumu yaliyokusudiwa.

Kwa upande wao baadhi ya Maafisa Ushirika, wameishukuru Serikali kwa kuwapatia usafiri hali itakayorahisha kuwatembelea wadau kwa urahisi tofauti na hapo awali, kutokana na baadhi ya maeneo wanayosimamia kiutekelezaji kuwa na tofauti kubwa ya umbali.

Pikipiki hizo aina ya Boxer, zimetolewa na Wizara ya Kilimo kupitia Tume ya Maendeleo na Ushirika kwa lengo la kurahisisha utendaji kazi  kwa Maafisa hao katika majukumu ya usimamizi wa vyama vya ushirika, ukaguzi,  utatuzi wa migogoro, usimamizi wa  masoko, uhamasishaji na utoaji wa mafunzo endelevu kwa wanachama,  viongozi na watendaji wa vyama vya Ushirika.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa