• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

RC ANDENGENYE ASHIRIKI CHAKULA CHA USIKU NA MASHUJAA FC

Posted on: May 24th, 2024

Washabiki na wadau wa Soka mkoani Kigoma wametakiwa kuzidi kuiunga mkono Timu ya  Mashujaa FC inayoshiriki Ligi Kuu ya Tanzania Bara (NBC Premier League) Msimu wa 2023/2024 ili iendelee kuwaletea Burudani wanakigoma sambamba na kutangaza fursa mbalimbali za kiuchumi zilizopo mkoani hapa.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye alipozungumza kwenye hafla fupi ya chakula cha usiku aliyoiandaa Mei 23, 2024  kwa lengo la kuwakutanisha pamoja wachezaji, viongozi pamoja na wadau wa Soka mkoani humo, ambapo amesisitiza kuwa pamoja na kutoa burudani kwa washabiki wa mchezo huo, Timu hiyo imekuwa na mchango mkubwa katika kutangaza vivutio vya utalii na uwekezaji vilivyopo mkoani Kigoma.

Aidha katika kuhakikisha timu hiyo inasalia Ligi Kuu msimu wa 2024/2025, mkuu huyo wa mkoa amewaalika washabiki wa mchezo huo ndani na nje ya Mkoa kujitokeza kwa wingi kwa lengo la kuwapa ari wachezaji ili iweze kuibuka na ushindi katika mechi zake mbili zilizosalia ambapo itakabiliana na Timu ya Mtibwa Sugar pamoja na Dodoma Jiji katika Dimba lake la nyumbani la Lake Tanganyika Stadium.

Upande wake Mwenyekiti wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Mkoa wa Kigoma (KFA) Alhaji Ahmed Mgoji amewakumbusha wachezaji wa Timu hiyo kufanya maandalizi ya kutosha  ili kuwakabili wapinzani wao na kushinda michezo iliyobaki ili kujiweka katika nafasi nzuri itakayowawezesha kuendelea kushiriki ligi kuu msimu wa 2024/2025.

‘’Michezo miwili iliyobaki tunacheza na timu zinazohitaji matokeo  kama ilivyo timu yetu ya Mashujaa, hivyo tunapaswa kupeana mikakati na makujumu ya pamoja ambayo tunapaswa kuyatekeleza ili kuhakikisha timu yetu inashinda na kubaki  ligi kuu ya Tanzania bara na kuendelea kuwaletea burudani washabiki wa mchezo huo.

Mwenyekiti wa Mashujaa FC Meja Abdul Tika amesema anaimani na kikosi chake kutokana na ubora wa wachezaji walionao sambamba na timu hiyo kuendelea kuimarika kila siku.

‘’ ligi ya Mwaka huu imekuwa ngumu kutokana na timu zote kutafuta nafasi muhimu ikiwemo nafasi ya pili pamoja na alama chache ambazo timu zimekuwa zikipishana hali inayoendelea kuifanya ligi kuwa ngumu hususani katika hatua za michezo ya mwisho ya ligi.

Naye Nahodha wa Kikosi hicho Maarufu kwa Jina la Mapigo na Mwendo Patrick Munthar amesema kutokana na nafasi waliyopo katika Ligi hiyo, jambo lililopo mbele yao ni kufanya bidi na kushinda michezo hiyo.

 ‘’Nikuahidi mheshimiwa Mkuu wa Mkoa tutashinda michezo iliyosalia, pia wachezaji wote wameona ni kwa kiasi gani unaguswa na kuwa karibu na Timu hii’’ alisisitiza Munthar


Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC SIRRO AZINDUA ZOEZI LA CHANJO NA UTAMBUZI WA MIFUGO KIMKOA

    July 03, 2025
  • JESHI LA UHAMIAJI KIGOMA LAPONGEZWA KATIKA KUKABILIANA NA WAHAMIAJI HARAMU

    June 23, 2025
  • MRADI WA BARABARA MWANDIGA KAGUNGA AWAMU YA KWANZA WAFIKIA 95%

    June 21, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA WAANZA KAMBI YA MATIBABU KIGOMA

    June 16, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa