• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

RC ANDENGENYE AONGOZA ZOEZI LA USAFI KUELEKEA MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI

Posted on: June 1st, 2024

Jamii imetakiwa kujenga utamaduni wa kufanya usafi na kutunza Mazingira katika maeneo wanayoishi ili kudumisha Afya na Mazingira bora ya kuishi.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye alipozungumza mara baada ya kuongoza zoezi la usafi ikiwa ni kuelekea maadhimisho ya Siku ya Mazingira duniani lililofanyika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Maweni Leo Juni 2024.

Amesema suala la uharibifu wa Mazingira limezidi kushika kasi mkoani hapa kutokana na baadhi wakazi kutotilia maanani umuhimu wa kutekeleza maelekezo ya serikali yanayohusu uhifadhi ikiwemo kutunza vyanzo vya maji, kutokata misitu ovyo pamoja na kufanya ufugaji na kilimo cha kisasa.

‘’Tuitumie siku hii kwa lengo la kukumbushana katika kuepuka kufanya shughuli za kibinadamu zinazoweza kuathiri vyanzo vya Maji, kupanda miti, kulinda maeneo yetu ya hifadhi za mazingira pamoja na kujifunza namna bora ya kuhifadhi au kutokomeza taka katika maeneo tunayoishi’’ amesisitiza Mkuu wa Mkoa.

Upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Dkt. Jesca Lebba amesema suala la usafi ni msingi wa kupunguza uwezekano wa milipuko ya maradhi mbalimbali na litasaidia katika kulinda Afya zetu.

Aidha amefafanua kuwa kampeni ya kuhimiza usafi kimkoa hususani ujenzi wa vyoo imefanikiwa kwa kiasi kikubwa ambapo mpaka kufikia mwaka 2024 uwepo wa vyoo kwenye kaya mkoani hapa umefikia asilimia 90.

Lengo la Maadhimisho haya ni kuhamasisha  umuhimu wa kulinda  na kuhifadhi Mazingira  pamoja na matumizi endelevu ya rasilimali za Mazingira ili kuleta  maendeleo endelevu duniani.

Ifahamike kuwa tarehe 5 Juni kila mwaka Tanzania huungana na Jumuia  kimataifa  kuadhimisha Siku ya Mazingira Duniani ikiwa ni moja wapo ya Maazimio  ya Mkutano wa Umoja wa Mataifa  kuhusu Mazingira na Maendeleo uliofanyika jijini Stockholm nchini Sweden mwaka 1972.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa