• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

RC ANDENGENYE AONGOZA KIKAO CHA TATU CHA KAMATI TENDAJI KiTiKi

Posted on: May 22nd, 2024

Zaidi ya wakulima 10,000 mkoani Kigoma wamepata mafunzo ya Kilimo Tija ili kuwawezesha kufanya Kilimo cha kisasa kwa lengo la kudhibiti uharibifu mkubwa wa Mazingira pamoja na kupata mazao ya kutosha kwa kutumia eneo dogo.

Hayo yamebainishwa kupitia taarifa iliyowasilishwa kwenye kikao cha tatu cha Kamati Tendaji ya usimamizi wa Mradi wa Kilimo Tija Kigoma (KiTiKi) kilichofanyika katika Hoteli ya Bwami Dubai Mjini Kasulu Leo Mei 22,2024.

Akizungumza mara baada ya kikao hicho Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye amesema Mradi wa KiTiKi unaosimamiwa na Shirika la Mpango wa Chakula la Umoja wa Mataifa (WFP) na kufadhiliwa na Shirika la Ushirikiano la Korea (KOICA) umelenga kuhakikisha wakimbizi wanaendelea kupata chakula kinachozalishwa nchini na kuwanufaisha wakulima wa ndani kupitia kilimo cha Maharage na Alizeti.

Amesema sambamba na kufanikisha kilimo cha mazao, Shirika hilo linatekeleza jukumu la kuwaunganisha wakulima wadogo na Taasisi za kifedha, kuwajengea uwezo ili waweze kuzalisha kwa tija, kuwaunganisha na masoko pamoja na kufanya kilimo cha kisasa na chenye udhibiti wa athari za kimazingira ikiwemo kuachana na kilimo cha kuhamahama.

Ameendelea kueleza kuwa, Kupitia mafunzo yanayotolewa na Programu hiyo, wakulima wanajengewa uwezo katika utunzaji bora wa mazao baada ya kuvuna, kuviimarisha vikundi vya kifedha vilivyoibuliwa miongoni mwao  pamoja na kuanzisha vituo vya ukusanyaji wa mazao na uuzaji ili kudhubiti wimbi la udalali linalochangia kiasi kikubwa kurudisha nyuma maendeleo ya wakulima.

‘’Kupitia vyama vya Msingi na AMCOS, Wakulima wataweza kuunganishwa na wanunuzi ili kupanga bei ya pamoja yenye tija kwa pande zote katika kuimarisha uchumi wa wakulima wadogo wadogo mkoani Kigoma’’amefafanua Andengenye.

Amesema mradi wa KiTiKi ni miongoni mwa miradi inayotekelezwa mkoani Kigoma chini ya Programu ya Pamoja ya Kigoma (UN Kigoma Joint Program) kwa sababu ni mojawapo ya eneo yenye jamii liyoathirika kwa kiasi kikubwa na ujio wa wakimbizi kutoka nchini Congo DR na Burundi na kusababisha wakazi wenyeji kupoteza maeneo yao ya asili huku mengine yakiathiriwa kwa kiasi kikubwa na uharibifu wa mazingira.

‘’ Programu hizi zinaendelea kutekelezwa mkoani hapa ili kuleta unafuu wa kimasiha kwa wakazi wenyeji ambao kwa ukarimu wao wameendelea kujitolea na kupoteza maeneo yao na rasilimali zao kwa ajili ya kuwatunza wenzao ambao wamekimbia nchi zao kutokana na ukosefu wa Amani’’amesisitiza Andengenye.

Upande wake Ihanjam Cha ambaye ni Afisa Mradi wa KiTiKi, amesema malengo ya mradi huo ni kusaidia upatikanaji wa chakula kwa wakimbizi pamoja na kuboresha mahusiano baina ya jamii ya wakimbizi na ile inayozunguuka kambi ambazo ni makazi ya wakimbizi hao.

Aidha amelitaja jukumu lingine la Taasisi hiyo isiyo ya kiserikali kuwa ni kuboresha maisha ya wakulima wadogo wadogo  katika wilaya  za Kasulu, Kibondo na Kakonko ambazo kwa namna moja au nyingine zimeathirika kwa kiasi kikubwa na uwepo wa jamii ya wakimbizi.

Naye Ali Mwembesazi ambaye ni Makamu Mkuu wa Ofisi ya WFP Kasulu amesema kupitia taasisi ya KiTiKi kwa Msimu wa 2023/2024 imefanikiwa kununua Tani 100 za maharage kutoka kwa wakulima mkoani Kigoma na kuyasambaza katika Kambi ya wakimbizi ya Nduta iliyopo wilayani Kibondo kuendana na malengo ya mradi.

Ameyataja mafaniikio mengine kuwa ni pamoja na kuwafikia wakulima 10,000 na kuwapatia mafunzo ya kilimo bora, uhifadhi wa chakula pamoja na kugeuza shughuli ya kilimo kuwa ajira  yenye tita.

‘’malengo yetu kwa mwaka 2024/2025 ni kuhakikisha tunawaunganisha wakulima na Taasisi za kifedha, kutoa mafunzo ya kilimo bora kwa wakulima wapya 10,000 kwa wilaya za Kasulu, Kibondo na Kakonko, ikiwa ni utekelezaji katika mwaka wa pili’’ amesisitiza.

Kupitia kikao chetu tumebaini kuwa changamoto kubwa ni upatikanaji wa mbegu ambapo kwa pamoja tumekubaliana kuandaa programu maalum kwa baadhi ya wakulima ambao ndio watakuwa wazalishaji kisha tukishathibitisha ubora wake tutazisambaza kwa wakulima.

‘’Aidha changamoto nyingine iliyojadiliwa ni pamoja na mabadiliko ya hali ya hewa hali inayosababisha kupunguza uzalishaji, suala ambalo tumekubaliana na maafisa ugani kushirikiana na wataalam wa hali ya hewa ili kutambua msimu stahili wa kilimo kuendana na mazao husika jambo litakaloepusha hasara kwa wakulima’’ amefafanua Ali.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AZINDUA RASMI ZOEZI LA UGAWAJI VYANDARUA KIMKOA

    May 27, 2025
  • JAMII INAPASWA KUZINGATIA CHANJO KUJILINDA NA MARADHI

    May 20, 2025
  • MRADI WA UHIFADHI MAZINGIRA WAZINDULIWA KIGOMA

    May 15, 2025
  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa