• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

RC ANDENGENYE AKAGUA MRADI WA MAJI MNANILA-NYAKIMWE

Posted on: May 29th, 2024

Wakazi mkoani Kigoma wametakiwa kujenga tabia ya kutunza maeneo ya vyanzo vya Maji ikiwemo kuepuka kufanya shughuli za kibinadamu pamoja na kupanda miti rafiki kwa mazingira ili kutoviathiri vyanzo hivyo na kuvifanya vidumu na kutoa huduma kwa muda mrefu.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye alipozungumza na wakazi wa wilaya ya Bihigwe alipokagua utekelezaji wa mradi wa Maji Mnanila-Nyakimwe na kusisitiza wakurugenzi wa Halmashauri kushirikiana na mamlaka za kimazingira katika vijiji  na mitaa katika kusimamia ulinzi wa vyanzo hivyo.

Amesema kumekuwa na changamoto katika maeneo meng ya mkoa kutokana na baadhi ya wananchi wasio waadilifu kupotosha wenzao kwa kuwahamasisha kutochangia huduma ya maji wakitoa sababu kuwa huduma hiyo ni ya bure ‘’ hii sio sahihi kwani kuna uhitaji mkubwa wa fedha kwa ajili ya gharama za ukarabati wa miundombinu na kuifanya kuwa endelevu’’ amesema Andengenye.

Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa mradi huo,  Meneja wa RUWASA Wilaya ya Buhigwe Mha. Golden Katoto amesema mradi wa maji Mnanila-Nyakimwe  unatekelezwa kwa Thamani ya Shilingi Bil. 9.7 ambapo utakapokamilika utahudumia wakazi 66,045 katika vijiji vya Bweranka, Kibande, Kitambuka, Nyakimwe, Mkatanga, Kibwigwa, Mnanila na Msagara wilayani humo.

Amesema hatua ya utekelezaji iliyofikiwa ni pamoja na ulazaji wa mabomba, ujenzi wa vituo kumi vya kuchotea maji, majengo ya mitambo, chemba 40 za kuondoa upepo, pamoja na ununuzi wa viungo vingine kwa ajili ya kuunganisha mfumo wa mabomba.

Sambamba na utekelezaji wa kazi hizo, Mhandisi Katoto amesema kazi zinazotarajiwa kuendelea kufanyika ni ujenzi wa matanki mawili ya kuhifadhia maji ambapo kila moja litakuwa na uwezo wa kuhifadhi lita 1,000,000.

Ameyataja matarajio ya RUWASA  mara baada ya kukamilika kwa mradi huo  ni pamoja na kuongeza huduma za upatikanaji wa maji kutoka Asilimia 72.2 hadi kufikia 90.2 ambapo mahitaji halisi ya maji katika vijiji hivyo ni lita1,660,125 huku ukitarajiwa kukamilika ifikapo Septemba 11, 2024.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa