• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENDEA KAZI KWA MAAFISA UGANI KILIMO

Posted on: August 19th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Thobias Andengenye ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kupitia Wizara ya Kilimo kwa kuendelea kufanya mageuzi makubwa kwenya Sekta ya Kilimo kwa lengo la kuwawezesha wakulima kufanya kilimo biashara chenye Tija.

Mhe. Andengenye ametoa kauli hiyo alipozungumza kwenye hafla ya kukabidhi vitendea kazi kwa maafisa Ugani Kilimo mkoa wa Kigoma na kusisitiza nyenzo hizo kutumika kwa malengo yaliyokusudiwa na Serikali.

Amesema sekta hiyo ni muhimu kwa ustawi wa Jamii mkoani Kigoma kutokana na zaidi ya Asimilia sabini ya wakazi kutegemea shughuli za kilimo kama chanzo chao kikuu cha uchumi kwa ajili ya kuendesha maisha yao ya kila siku.

‘’Pamoja na Mchango mkubwa wa sekta hiyo katika mkoa wa Kigoma bado wakazi wanafanya kilimo cha kujikimu hivyo dhamira ya serikali ni kufanya mageuzi makubwa kutoka aina hiyo ya Kilimo na kuingia katika mfumo wa kilimo biashara’’ amesema Andengenye.

Kupitia hafla hiyo, mkuu huyo wa Mkoa amegawa magari mawili(2)yaliyotolewa na Wizara ya Kilimo kwa ajili ya kuratibu shughuli za kilimo ngazi ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na katika Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe pamoja na mavazi 179 kwa ajili ya Maafisa Ugani Kilimo ngazi ya Mkoa na Halmashauri.

Aidha Mhe. Andengenye amezikumbusha halmashauri kutekeleza maagizo ya Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe ikiwemo halmashauri ya Kigoma Ujijiku kutenga eneo ili wizara hiyo iweze kutekeleza mradi wa ujenzi wa Kituo cha kuratibu shughuli za umwagiliaji nchini.

Sambamba na agizo hilo, Andengenye ameitaka halmashauri ya wilaya ya Kibondo kutekeleza agizo la kutenga eneo ili serikali iweze kutekeleza mradi wa ujenzi wa soko la kisasa la zao la muhogo huku halmashauri ya Buhigwe ikitakiwa kuandaa eneo kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda cha kuchakata zao la Tangawizi.

Aidha Mhe Andengenye amezielekeza halmashauri zote za mkoa kutenga maeneo ya ujenzi wa masoko ya kimkakati  kwa ajili ya kuwawezesha wananchi kuyafikia masoko hayo na kufanya biashara za mazao yao mazao ya kilimo kwa faida.

Katika hatua nyingine Mhe. Andengenye amekabidhi fedha Taslim kiasi cha Shilingi Mil. 1 kwa niaba ya Waziri wa Kilimo kwa Afisa Ugani Kilimo Manispaa ya Kigoma Ujiji Bi. Sarah Micheal  kufuatia waziri huyo kufurahishwa na usimamizi mzuri wa shughuli za kilimo alioufanya mtendaji huyo katika bonde la mto Luiche mkoani hapa.    


Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa