• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

RC ANDENGENYE AKABIDHI MSAADA KWA WAATHIRIKA WA MAFURIKO HALMASHAURI ZA KIGOMA UJIJI, KIGOMA NA UVINZA

Posted on: October 22nd, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Thobias Andengenye amewashukuru wadau wa Maendeleo wa Mkoa wa Kigoma ikiwemo mashirika na Taasisi Binafsi zinazofanya shughuli zake mkoani Kigoma kwa kuendelea kuigusa jamii ikiwemo kutoa misaada mbalimbali ya kiutu kwa lengo la kuunga mkono juhudi za serikali katika kuwaondoloea adha wananchi.

Mhe. Andengenye ametoa Kauli hiyo alipozungumza kwenye hafla fupi ya kugawa vifaa vilivyotolewa na Shirika la kuhudumia watoto duniani (UNICEF) kwa ajili ya kusaidia waathirika wa mafuriko yaiyosababishwa na mvua nyingi zilizonyesha mkoani Kigoma kati ya Desemba 2023 hadi Aprili 2024 hususani katika Halmashauri za Kigoma Ujiji, Uviza na Kigoma.

Amewataka wakuu wa wilaya za Uvinza, Kigoma na Manispaa ya Kigoma Ujiji ambazo zimepokea vifaa hivyo kuhakikisha vinawafikia walengwa na kuwanufaisha kama ilivyokusudiwa sambamba na kuwataka wananchi kuepuka kujenga katika maeneo ya mabondeni ili kuepuka athari zitokanazo na mvua jambo linaloweza hatarisha usalama wa maisha na mali zao.

Upande wake Mkuu wa Ofisi ya Shirika la UNICEF Kigoma Justus Ndenzako amesema vifaa vilivyokabidhiwa kwa wakuu wa wilaya hizo kwaniaba ya wahitaji ni pamoja na Magodoro 200, ndoo 300, blangeti 310, vyandarua 100 pamoja na mashuka 10 vyote vikiwa na Thamani ya zaidi ya Shilingi Mil. 20

Amefafanua kuwa, shirika la UNICEF linatoa linaendelea kushirikiana na Serikali katika kutekeleza miradi mbailmbali ya kijamii ikiwemo ile iliyopo katika Sekta zinazohusisha utoaji wa huduma za jamii, hivyo kutoa misaada hiyo ni mojawapo ya sehemu ya utekelezaji wa kazi zinazoguza jamii moja kwa moja.

Mkuu wa wilaya ya Uvinza Mhe. Dinah Mathamani ameushukuru uongozi wa shirika hilo na kuahidi kufikisha misaada hiyo moja kwa moja kwa walengwa.

Hadi kufikia Mwezi Juni 2023 jumla ya Kaya 411 zilithibitika kukosa makazi katika Halamshauri za Uvinza, Kigoma na Manispaa ya Kigoma Ujiji, huku jumla ya wakazi 3,419 waihama makazi yao kutokana na athari za Mvua zilizonyesha mkoani Kigoma.


Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AZINDUA RASMI ZOEZI LA UGAWAJI VYANDARUA KIMKOA

    May 27, 2025
  • JAMII INAPASWA KUZINGATIA CHANJO KUJILINDA NA MARADHI

    May 20, 2025
  • MRADI WA UHIFADHI MAZINGIRA WAZINDULIWA KIGOMA

    May 15, 2025
  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa