• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

RC ANDENGENYE AKABIDHI BAISKELI 250 KWA WAHUDUMU WA AFYA NGAZI YA JAMII

Posted on: August 20th, 2024

Wahudumu wa Afya ngazi ya Jamii Mkoani Kigoma wameishukuru serikali kwa kuendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa Sekta ya Afya ili kuweka mazingira rafiki yanayowezesha michango ya wadau hao kuigusa jamii kwa kurahisisha utoaji na upatikanaji wa Huduma.

Wakizungumza mara baada ya kukabidhiwa baiskeli ikiwa ni ufadhili kutoka Shirika lisilo la kiserikali Catholic Relief  Services (CRS) kwa ajili ya kurahisisha utuatiliaji na utoaji wa huduma, baadhi ya wanufaika wa nyenzo hizo za usafiri wamesema kupatikana kwa vitendea kazi hivyo kutasaidia kuifikia namba kubwa ya wateja wao na kwa wakati sahihi.

Honorina Sunzu ambaye ni muhudumu wa Afya ngazi ya Jamii kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma anasema awali walikuwa wakitumia muda mrefu kuwafikia walengwa jambo lililosababisha baadhi yao kushindwa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

‘’Nyenzo hizi zimeamsha ari katika utendaji kazi wetu, hivyo tunaishikuru serikali kwa kushirikiana na wadau wa Afya kwa kuiona changamoto hii iliyokuwa ikitukabili kisha kuamua kuitatua’’ amesema.

Mkuu wa Shirika lisilo la kiserikali la Catholic Relief Services Tanzania (CRS) Taylor Lanton amesema Shirika hilo limetoa Baiskeli 250 ambapo kati ya hizo 200 ni kwa ajili ya wahudumu wa Afya ngazi ya Jamii pamoja na walimu wa Vijiji kwa ajili ya vikundi vya kuweka na kukopa vijijini ili kuwaaezesha kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Amesema mojawapo ya majukumu ya msingi ya Shirika hilo ni kutekeleza mradi unaolenga kuboresha hali za afya na lishe kwa vijana walio katika rika balehe waliopo shuleni na kwenye Jamii sambamba na wanawake vijana wenye umri kati ya miaka 10 hadi 24 mkoani Kigoma.

‘’Tunaendelea kuangalia zaidi katika kuiongezea nguvu serikali katika kuboresha Afya ya Jamii, uwepo wa lishe bora sambamba na kuboresha maisha ya mtu mmoja mmoja kupitia maeneo hayo, aidha nimefurahishwa na namna mnavyoutekeleza mradi pamoja na ushirikianomkubwa mnaotupa kama uongozi wa mkoa wa Kigoma nasi tunaendelea kuahidi kufanya kazi nanyi’’ amesema Bi. Lyton.

Akizungumza kabla ya kukabidhi vitendea kazi hivyo Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Thobias Andengenye amesema  Serikali ya awamu ya Sita kupitia wizara ya Afya itaendelea kushirikiana na wadau wa Maendeleo kupitia sekta hiyo ili kukabialiana na changamoto zinazowakabili wananchi hususani katika upatikanaji wa huduma bora za Afya.

Amewataka wanufaika wa vitendea kazi hivyo kwenda kuvitumia kuendana na miongozo waliyopewa ili viweze kuleta ufanisi katika Mapinduzi ya Sekta hiyo muhimu  sambamba na kupunguza idadi ya vifo vya wanawake wajawazito na watoto katika maeneo ya vijijini.

 ‘’Nichukue nafasi hii kuwashukuru na kuwapongeza wahudumu wote wa Afya ngazi ya Jamii mkoa wa Kigoma kwa kazi nzuri mnazozifanya ambazo zimekuwa na mchango mkubwa katika kuboresha Afya, lishe na Ustawi wa watu wa Kigoma kwa jumla’’amesisitiza Andengenye.

Jumla ya baiskeli 72 zimegawiwa katika halmashauri ya Kigoma, 84 Wilaya ya Uvinza na nyingine 94 zikitolewa kwa wanufaika katika halmashauri ya wilaya ya Kibondo.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa