• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

RC ANDENGENYE AIPONGEZA MAHAKAMA KIGOMA KWA KUIMARISHA MATUMIZI YA TEHAMA

Posted on: January 27th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye ameipongeza Serikali kupitia Sekta ya Sheria Nchini kwa kuimarisha matumizi ya Mfumo wa TEHAMA katika kutoa Huduma za kimahakama, hali inayoongeza kasi na kurahisisha mchakato wa kutoa haki kwa wananchi.

Andengenye ametoa kauli hiyo alipozungumza kwenye maadhimisho ya wiki na Siku ya Sheria nchini yaliyofanyika kimkoa katika viwanja vya Mwana Centre, Manispaa ya Kigoma Ujiji ambapo amewataka wananchi kutumia fursa ya uwepo wa maadhimisho hayo kupata Elimu na misaada ya kisheria.

Amesema kuimarika kwa mifumo ya utoaji wa huduma za kisheria kumeendelea kuchangia kuimarisha uchumi wa mkoa Mkoa kwani Maendeleo hutegemea mahitaji makubwa ya kiwango cha haki jambo linaloendelea  kuvutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi.

Katika hatua nyingine Andengenye amewataka watumishi wa Mahakama mkoani Kigoma kuendelea kutoa Huduma bora za kisheria kwa kuzingatia wakati ili kuruhusu wananchi kupata muda wa  kushughulikia masuala ya kimaendeleo.

‘’Mahakama pekee haiwezi kutoa haki kama wadau wake hawajajipanga na kuboresha mnyororo wote wa utoaji wa Huduma za kisheria’’ amesisitiza Mkuu wa Mkoa.

Awali akimkaribisha Mkuu wa Mkoa, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma Mhe. Augustine Rwizile amesema Serikali inaendelea kuboresha mfumo wa Mahakama mtandao ili kurahisisha na kuimarisha utoaji wa Huduma za kimahaka.

‘’Mahakama imeendelea kutumia mifumo ya kiteknolojia kushughulikia mashitaka mbalimbali kwani kuanzia Novemba 2023,  tumekuwa tukitumia mfumo mpya wa Usimamizi wa Kesi, ambapo unawezesha kusajili mashitaka, kupangiwa tarehe na hatimaye kusikilizwa’’amesema Jaji Rwizile.

Maadhimisho ya Wiki na Siku ya Sheria yameanza Januari 24, 2024 na yanatarajiwa kuhitimishwa kwa kufikia kilele chake Februari 1, 2024, yakibeba Kauli Mbiu isemayao  ‘’umuhimu wa dhana ya Haki kwa ustawi wa Taifa, nafasi ya wadau na Mahakama katika kuboresha Mfumo Jumuishi wa Haki Jinai’’

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa