• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

RC ANDENGENYE AHUTUBIA KONGAMANO LA 34 CHUO KIKUU HURIA TANZANIA

Posted on: December 4th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thpbias Andengenye ameupongeza Uongozi wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT TZ) kwa kutoa ufadhili wa nusu ya ada kwa walimu wa shule za Umma jambo lililochangia kwa kiasi kikubwa kuboresha Taaluma ya watendaji katika kada hiyo.

Kauli hiyo imetolewa na Kiongozi huyo alipohutubia Kongamano la 34 la wanazuoni wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania lililofanyika katika Kituo cha chuo hicho cha Mkoa wa Kigoma kuelekea Mahafali ya 43 ya chuo yanayotarajiwa kufanyika Desemba 5, 2024 mkoani humo.

Kupitia hotuba yake Andengenye amekipongeza chuo hicho kwa kudumisha mahusiano na taasisi za kitaaluma za ndani na nje ya nchi kwa lengo la kubadilishana utaalam, kufanya tafiti pamoja na  kuendesha miradi mbalimbali ya pamoja kwa lengo la kuimarisha utoaji wa taaluma kwa wanafunzi wa chuo hicho.

Andengenye amewapongeza wahitimu wote wanaotarajiwa kutunukiwa kutokana na kuhitimu ngazi mbalimbali za kitaaluma na kuwasisitiza kutoishia hatua walizofikia.

Ameongeza kwa kutoa wito kwa wahitimu hususani walio katika mifumo ya kuajiriwa na kujiajiri kwenda kuongeza ufanisi katika utendaji kazi wao ili waweze kujitofautisha na kuwa wahitimu shindani katika soko la ajira.

Prof. Carlolyne Nombo Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu kwa kuendelea kuwekeza katika ngazi zote za kielimu ili kuleta  ufanisi katika elimu Msingi, Sekondari na ngazi za vyuo.

Prof. Nombo ameupongeza uongozi wa chuo kwa kuzalisha wataalam wengi na wenye elimu bora,  kwani elimu inayotolewa na chuo hicho inawapa fursa wahitimu kuitumia ndani na nje ya nchi na kuleta matokeo chanya.

"Ninaamini kupitia uzoefu wa kutekeleza mfumo wa elimu nyumbuifu mtaelekeza na kutoa ushauri kwa Wizara ya Elimu ili kupata namna ya kutoa elimu kwa utaratibu huo katika ngazi mbalimbali za kielimu nchini" amesema.

Amesisitiza kuwa, Wizara itaendelea kufanya kazi kwa karibu ikiwa kutekeleza miradi ya kimkakati ikiwemo utekelezaji mradi wa HEET unaolenga kuimarisha Utawala, Miundombonu na kujenga misingi ya elimu.

"Mradi wa HEET umejielekeza kujenga maabara ya kisasa ya Sayansi mkoani Kigoma jambo, litakalokuwa fursa kwa wanafunzi wa kituo cha Kigoma na maeneo jirani kusoma kwa vitendo zaidi" amesisituza Prof. Nombo.

Aidha ameusisitiza uongozi wa mkoa kufanya ufuatiliaji wa karibu ili kuhakikisha ujenzi wa Maabara hiyo unakamilika ndani ya muda uliopangwa.

Niwaahidi wizara kufanya kazi kwa karibu ili kuhakikisha dhamira ya Chuo Kikuu Huria  ya kutoa elimu kwa njia ya masafa ikiwemo elimu ya juu inaendelea kufanyika kwa ufasaha.


Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa