• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

RC ANDENGENYE AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA WATENDAJI MIRADI YA BOOST

Posted on: September 25th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye amewasisitiza  watendaji wa Serikali mkoani Kigoma kusimamia utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo kwa umakini na uadilifu ili kutokuwa kikwazo kwa Serikali katika kupeleka Maendeleo kwa wananchi.

Mkuu huyo wa Mkoa ametoa maelekezo hayo akiwa katika ziara ya kutembelea na kukagua utekelezaji wa Miradi ya BOOST na SEQUIP katika Halmashauri ya Mji Kasulu, huku akisisitiza suala la ufuatiliaji na kufanya tathimini `wakati wote wa utekelezaji wa miradi hiyo.

Amesema watendaji wanapaswa kuepuka kuzipa nafasi changamoto na kuwa sababu au vigezo vya kushindwa kufikia malengo yaliyowekwa na serikali, bali watoe taarifa kwa ngazi nyingine za kiserikali ili kupata utatuzi wa vikwazo vinavyojitokeza wakati wa utekelezaji.

‘’Tumepewa nafasi hizi za usimamizi serikalini ili kubaini na kutatua changamoto  zinazoleta ukinzani katika kufanikisha hatua mbalimbali zitakazowezesha maendeleo kuwafikia wananchi, hivyo tusiogope kukabiliana nazo na huo ndio wajibu wetu mkubwa’’ amesema Andengenye.

Ameendelea kusisitiza kuwa, watendaji hawana sababu ya kushindwa kukamilisha miradi ya maendeleo wakati serikali inapeleka fedha za kutosha katika maeneo inakotekelezwa miradi hiyo.

Kupitia ziara hiyo Mkuu wa Mkoa ametembelea na kukagua utekelezaji wa miradi ya Ujenzi wa miundombinu mbalimbali kwa ajili ya uboreshaji wa Mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji chini ya program za BOOST na SEQUIP katika Shule ya Sekondari Nyumbigwa Mpya, Muka, Msambara pamoja na Shule za Msingi Kasulu, Nyasha na Kibagwe.

Aidha kukamilika kwa miradi hiyo kunatarajia  kupunguza mrundikano wa wanafunzi madarasani,  vyooni pamoja na kupunguza umbali kwa wanafunzi kuyafikia maeneo hayo ya huduma za kitaaluma.

Pia baadhi ya wakazi wanaoishi katika maeneo inakotekelezwa miradi hiyo wametanabaisha kunufaika kwao kutokana na miradi hiyo kuchangia upatikanaji wa ajira za muda zinazowasaidia kupata fedha kwa ajili ya kujikimu kimaisha.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa