• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

RC ANDENGENYE AHIMIZA HUDUMA YA CHAKULA SHULENI

Posted on: January 20th, 2023

PICHA: Kikao cha Tathimini ya utekelezaji wa shughuli za uboreshaji na usimamizi wa Elimu Mkoa wa Kigoma Kilichofanyika  Januari 20, 2023 katika Ukumbi wa NSSF mANISPAA YA Kigoma-Ujiji.

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma  Kamishna Jenerali Mstaafu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mhe. Thobia Andengenye amewataka wazazi na wadau wa Elimu kuhakikisha Huduma ya Chakula inaanza kutolewa kwa Shule zote za Msingi na Sekondari katika Mkoa wa Kigoma ili kuimarisha utulivu na usikivu wakati wa utekelezaji wa zoezi la ujifunzaji na ufundishaji.

Melekezo hayo ameyatoa Leo Januari 20, 2023 alipomwakilisha Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mhe. Angellah Kairuki kwenye Kikao Kazi cha Tathimini ya Utekelezaji wa Shughuli za Uboreshaji na Usimamizi wa Elimu Mkoa wa Kigoma kilichowakutanisha Viongozi na Watendaji wa Sekta ya hiyo mkoani Kigoma.

‘‘Kila Mzazi anajukumu la kutoa chakula cha kila Siku katika Familia hivyo sioni sababu ya wazazi kushindwa kutekeleza jukumu hilo muhimu kwa manufaa ya watoto wao ili waweze kupata Afya bora. Pia ikumbukwe, ulishaji wa wanafunzi shuleni utatupunguzia changamoto ya utapiamlo na udumavu Mkoani kwetu na Taifa kwa ujumla’’ amesema Andengenye.

Kwa Mujibu wa Taarifa ya Mapitio ya Tathimini ya utekelezaji wa Shughuli za Uboreshaji na usimamizi wa Elimu Kimkoa, hadi kufikia Januari 19,2023 Idadi ya Shule za Msingi zinazotoa Huduma ya Chakula shuleni kimkoa ni shule 43 kati ya 218 na upande wa  Sekondari ikiwa 156 kati ya 708.

Akitoa Taarifa ya Mapitio ya Tathimini ya Utekelezaji wa Mikakati ya Kuboresha Elimu Msingi na Sekondari kwa Mwaka 2022 kwa niaba ya Katibu Mkuu OR-TAMISEMI, Katibu Mtendaji Tume ya Utumishi wa Walimu  Taifa Bi. Paulina Nkwama amesema lengo la kikao kazi hicho ni kujenga uelewa wa pamoja kuhusu namna  ya kutekeleza mikakati na utatuzi wa Changamoto zilizobainishwa katika  miongozo ya elimu pamoja na kutoa hamasa kwa viongozi, wasimamizi na walimu katika kutekeleza Majukumu yao.

Amefafanua kuwa, Ofisi ya Rais TAMISEMI iliweka vigezo vya Upimaji  wa Utendaji kazi kwa ngazi mbalimbali za Uongozi na watendaji katika Tasnia ya Elimu ili kuhakikisha Changamoto za kiutendaji zilizobainika  katika Mwaka 2022 zinapatiwa ufumbuzi wa kudumu.

‘’Nasisitiza kila mshriki wa kikao kazi hiki atoke na uelewa wa kutosha kuhusu majukumu yaliyoko mbele yake na namna atakavyojipanga ili kufikia malengo yaliyobainishwa katika Miongozo ya Uboreshaji na Usimamizi wa Elimu katika Ngazi zote’’ amesisitiza Nkwama.

Upande wake Afisa Elimu Mkoa wa Kigoma. Paulina Ndigeza amesema hali ya uandikishaji kwa Wanafunzi waliofaulu Drasa la Saba na kutakiwa kuanza Kidato cha Kwanza  kwa Muhula wa Masomo 2023 imefikia Asilimia 58.4

‘‘Hadi kufikia Tarehe 19, Januari 2023 Mkoa wa Kigoma kupitia Idara ya Elimu tumefanikiwa kuandiskisha Wanafunzi 12,781 wanaotakiwa kuanza Kidato cha Kwanza ambapo wavulana na 13,019 na Wasichana 12,762 ambapo ni sawa na Asilimia 58.4 ya Wanafunzi wote waliotakiwa kujiunga na Elimu ya Sekondari kwa Mkoa wetu’’ amesema Ndigeza.

 Aidha kupitia kikao hicho Muhimu cha wadau wa Elimu mkoani Kigoma wajumbe wameazimia kuwa, wazazi, Uongozi wa Elimu na Serikali pamoja na watendaji wa Idara hiyo, kufuatilia na kuhakikisha wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza wawe wameandikishwa ifikapo tarehe 31, Januari 2023.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa