• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

RC AHIMIZA UWAJIBIKAJI KATIKA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

Posted on: January 13th, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Kamishna Jenerali Mstaafu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mhe. Thobias Andengenye amewataka watendaji wa Serikali kusimamia miradi inayotekelezwa na Serikali kwa ukaribu na umakini mkubwa ili iweze kukamilika kwa wakati na kiwango sahihi kuendana na miongozo ya   Serikali.

Mkuu wa Mkoa ametoa Melekezo  hayo alipofungua kikao kazi cha  Tathmini ya utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo kwa Mwaka 2022/2023 kwa Mkoa wa Kigoma, kilichowakutanisha Wakuu wa wilaya, Makatibu Tawala wilaya, Wakurugenzi, pamoja na wakuu wa Idara na Vitengo  katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma.

‘‘Ipo changamoto kwa baadhi ya watendaji wenye dhamana kutosimamia  kwa ukaribu Miradi ya Maendeleo inayotekelezwa na serikali na kusababisha baadhi ya kazi kutofanyika kwa kuzingatia Miongozo na Maelekezo yanayotolewa na Serikali, hali inayoweza kusababisha  baadhi ya miradi  kutekelezwa chini ya kiwango  au kinyume na miongozo ya Serikali’’ amesema Andengenye.

Ameendelea kusisitiza kuwa, watendaji waache kuorodhesha changamoto na kuzitumia kama kisingizio cha kutotekeleza Miradi kwa ufasaha na kwa wakati uliopangwa, bali wajikite katika usimamizi wa karibu na kuikagua miradi hiyo mara kwa mara huku  wakizingatia miongozo inayotolewa na Serikali katika utekelezaji wa kazi hizo.

Naye Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma Albert Msovela amewataka wakuu wa vitengo  vya Manunuzi katika Halmashauri kuongeza ufanisi na kuzingatia muda katika kufanya manunuzi ya vifaa vya ujenzi ili  kuharakisha utekelezaji wa shughuli za maendeleo mkoani Kigoma.

Amesisitiza kuwa, vitengo vya Manunuzi katika maeneo mengi vimekuwa changamoto katika kuhakikisha manunuzi yanafanyika katika muda uliopangwa hali inayosababisha  miradi mingi inayotekelezwa  kutokukamilika kwa wakati.

Pia amewaasa watendaji wa Serikali kuongeza ushirikiano na kudumisha mahusiano mema katika utendaji kazi ndani ya Mkoa jambo litakalorahisisha uwepo wa mawasiliano ya karibu na kufikiwa kwa malengo ya kiutendaji.

Upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Ester Mahawe amewashauri wakurugenzi na wakuu wa Idara na vitengo vinavyosimamia utekelezaji wa kazi za Maendeleo kutembelea mara kwa mara maeneo ya utekelezaji ili waweze kubaini dosari zinazojitokeza na kuzifanyia kazi kwa wakati kabla ya kukamilika kwa miradi hiyo.

‘‘Namna bora ya kudhibiti changamoto katika miradi yetu tunayoitekeleza ni kuhakikisha miongozo na Maelekezo yanayotolewa na Serikali yanazingatiwa. Baadhi ya watendaji katika maeneo ya utekelezaji wamekuwa wakifanya kazi kinyume na taratibu, ili kudhibiti mapungufu yanayoweza kujitokeza  suluhisho ni kufanya ukaguzi wa mara kwa mara na kutoa maelekezo kuendana na miongozo ya Serikali’’ amesema Mahawe.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa