• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

RAS RUGWA ATOA SIKU 14 KITUO CHA AFYA KAJANA KUANZA KUTOA HUDUMA

Posted on: May 17th, 2024

Wakazi wilayani Buhigwe Mkoani hapa wameiomba Serikali kuendelea kusimamia ahadi inazozitoa katika utekelezaji wa miradi ya Maendeleo ili iweze kukamilika kwa wakati na kuondoa adha kwa wananchi.

Kauli hiyo imekuja kufuatia agizo la Katibu  Tawala Mkoa wa Kigoma Hassan Rugwa kumtaka Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe kuhakikisha Kituo  cha Afya Kajana kilichoanza ujenzi wake Mwaka 2021 kinafunguliwa na kuanza kutoa Huduma ifikapo Mei 28, 2024.

Amesema serikali haitomvumilia mtumishi yeyote wa Umma atakayebainika kukwamisha utekelezaji wa Maagizo maelekezo ya usimamizi wa Miradi kwani hali hiyo inasababisha migogoro baina ya wananchi na serikali yao sambamba na kuchelewesha maendeleo.

Amesema wenye jukumu la usimamamizi wa miradi hiyo  wanapaswa kujitathmini huku akisisitiza  kuwa iwapo kuna mtendaji wa serikali anabainika  atasababisha mkwamo katika utekelezaji wa miradi ya kutolea huduma kwa wananchi, Serikali haitosita kumchukulia hatua.

Sambamba na hilo, Katibu Tawala huyo amesema agizo hilo linapaswa kwenda sambamba na ukamilishwaji wa miundombinu ya Nyumba za watumishi, tanki la Maji pamoja na choo katika Zahanati ya Kijiji Kasumo, ili kuruhusu wananchi kupata huduma za kiafya katika maeneo ya jirani na makazi yao.

Upande wake Mganga mkuu wa Mkoa wa Kigoma Jesca Lebba amesema Ofisi yake imepokea maelekezo hayo hivyo itashirikiana na Ofisi ya  Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo ili kuhakikisha huduma za Afya zinaanza kutolewa katika maeneo yaliyoelekezwa ifikapo Mei 28,2024.

‘’Tunaahidi kuhakikisha tunaleta hapa wataalam wa Afya pamoja na vifaa vya kuanzia hususani katika jengo la wagonjwa wa nje ili ifikapo Mei 28,2024 huduma za msingi za awali zianze kutolewa wakati tunaendelea kukamilisha uwekaji wa vifaa kwa ajili ya utoaji wa huduma kubwa kama zile za upasuaji’’ amesema Lebba.

Akitoa ufafanuzi kuhusu changamoto zinazosababisha kuchelewa kwa ujenzi huo, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Ugavi na Manunuzi katika Halmashauri hiyo Godwin Nsemwa amesema kumekuwa na changamoto ya manunuzi ya vifaa kutokana na kuhcelewa kwa michakato ya kuwapata wazabuni kwa ajili ya kuiuzia Halmashauri zana za ujenzi.

Upande wao baadhi ya wakazi wa kijiji hicho wamesema watendaji wa Halmashauri hiyo wameshindwa kuishirkisha kwa ufasaha kamati ya manunuzi na badala yake wamekuwa wakijichukulia maamuzi bila kuishirikisha kamati hiyo hali inayowafanya kushindwa kufahamu msingi wa kutofikiwa kwa malengo ya ujenzi.

‘’Ujenzi wa Kituo hiki cha Afya ulianza kwa hatua za awali mwaka 2021 mara baada ya Halmashauri kupokea kiasi cha shilingi mil.500 lakini mpaka sasa kazi mbalimbali zimeendelea kusuasua hali inayotupa changamoto ya kupata huduma bora za kiafya kutokana na huduma hizo kupatikana maeneo ya mbali’’alisema Januari Luckas Mkazi wa Kajana wilayani humo.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa