• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

RAS RUGWA AAGIZA WAKURUGENZI KUHUISHA ZOEZI LA UPATIKANAJI WA HATI MILIKI KWA MAENEO YA SERIKALI

Posted on: May 27th, 2024

Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma Hassan Rugwa amewaelekeza wakurugenzi watendaji wa Halmashauri nane za Mkoa wa Kigoma kuhuisha zoezi la kupima na kuandaa hati miliki kwa ajili ya maeneo yote yanayomilikiwa na  Serikali mkoani Kigoma.

Rugwa ametoa maelekezo hayo akiwa kwenye ziara ya ukaguzi wa utekelezaji miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya wilaya ya Kasulu na kusisitiza kuwa utekelezaji wa agizo hilo utapunguza uwepo wa migogoro ya Ardhi baina ya Serikali na wananchi wanaovamia maeneo yanayomilikiwa na Taasisi za Umma.

Amesema ukosefu wa hati miliki katika maeneo ya Taasisi za Umma imekuwa ni changamoto ya mudamrefu katika halmashauri na kusababisha upotevu mkubwa wa Fedha na muda kutokana na ufuatiliaji wa mashauri hayo katika  ngazi mbalimbali za kimahakama.

‘’Nitumie nafasi hii kutoa maelekezo haya kwa wakurugenzi ili waweze kuwaelekeza na kuwasimamia viongozi wote wa Taasisi za Umma kushirikiana na wataalam wa Ardhi kwa lengo ya kuyatambua maeneo tengefu au yale yenye miundombinu kisha kuyaandalia utaratibu wa kuyawekea hati miliki hizo’’ amesisitiza Rugwa.

Amesema serikali inawekeza kiasi kikubwa cha fedha katika ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya Umma hivyo kukosekana kwa hati katika maeneo hayo ni sawa na kushindwa kuheshimu juhudi za serikali katika kutoa huduma na kuyaweka katika hatari ya kuvamiwa na kusababisha migogoro isiyokuwa ya lazima.

Aidha Rugwa amesisitiza kuwa halamshauri zote zinatakiwa kuanza kutekeleza agizo hilo kuanzia Julai Mosi, 2024 ambapo katika kipindi cha miezi mitatu kuanzia tarehe hiyo, kila taasisi za Umma katika halmashauri hizo itatakiwa kuwa imekamilisha zoezi hilo.

Albert Mhoza mkazi wa Kijij cha Chekenya wilayani Kasulu amesema iwapo serikali itatekeleza zoezi hilo la kuyapima na kuyawekea hati miliki maeneo hayo, itapunguza migogoro ya ardhi na wananchi kwani tabia ya uvamizi hutokana na maeneo mengi kukosa utambulisho wa umiliki wa serikali pamoja na kutoendelezwa kwa muda mrefu.

‘’Maeneo ya Taasisi za kielimu na Afya zimekuwa zikiongoza kwa watu kuvamia maeneo hayo na kutumia rasilimali zilizopo ikiwemo uharibifu wa hifadhi za mazingira ikiwa  ni pamoja na ukataji wa miti na uharibifu wa miundombinu inayotumika kwa ajili ya kutoa huduma kwa jamii’’ amesisitiza.

Aidha kupitia ziara hiyo Katibu Tawala amewasisitiza watendaji katika halmashauri ya Kasulu kuongeza kasi katika kusimamia miradi ya Maendeleo ili iweze kukamilika kwa wakati na kutoa huduma bora kwa wananchi.

Katika ziara hiyo, Kiongozi huyo ametembelea na kukagua ukamilishwaji wa jengo la upasuaji katika Hoapitali ya Wilaya ya Kasulu, jengo la Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri pamoja na ujenzi wa Zahanati ya Chekenya.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • JESHI LA UHAMIAJI KIGOMA LAPONGEZWA KATIKA KUKABILIANA NA WAHAMIAJI HARAMU

    June 23, 2025
  • MRADI WA BARABARA MWANDIGA KAGUNGA AWAMU YA KWANZA WAFIKIA 95%

    June 21, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA WAANZA KAMBI YA MATIBABU KIGOMA

    June 16, 2025
  • MRADI WA UHIFADHI MAZINGIRA WAZINDULIWA KIGOMA

    May 15, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa