• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

RAIS SAMIA APONGEZWA UJENZI WA MADARASA YA KIDATO CHA KWANZA 2023

Posted on: December 13th, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Thobias Andengenye amempongeza Mhe Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa maamuzi sahihi ya kutoa Fedha zaidi ya Shilingi Bil. 7.61 kwa ajili ya Ujenzi wa Vyumba 358 vya Madarasa kwa Mkoa wa Kigoma kwa ajili ya wanafunzi wanaotarajia kuanza kidato cha kwanza Mwaka 2023.

Fedha hizo zilizotolewa na Mhe. Rais,  zimelenga kumpunguzia mzigo wa michango mwananchi wa kawaida na kuhakikisha kila Mwanafunzi aliyefaulu Elimu ya Msingi, anajiunga na kuendelea ngazi ya Sekondari bila kuwepo kwa changamoto hiyo ambayo hapo awali imechangia kiasi kikubwa katika kuathiri na kushusha ufanisi katika Taaluma.

Andengenye ametoa pongezi hizo huku akisisitiza wanaofanya kazi za ujenzi wa madarasa hayo watangulize uzalendo kwa kuhakikisha kazi wanazozifanya zinaakisi Thamani halisi ya Fedha zilizotolewa na Mhe. Rais

‘‘Ili tuonyeshe ni kwa kiasi gani sote tunathamini maamuzi ya Rais wetu, tutangulize uzalendo kwa kuwa waadilifu katika matumizi ya fedha hizo pamoja na kuhakikisha kazi zinazofanyika zinalingana na Thamani ya fedha zilizotolewa’’

‘‘Hapa tunajenga chetu kwa manufaa yetu na kizazi chetu, hivyo hakuna haja ya kufanya udanganyifu wa aina yoyote na atakayefanya hivyo ajue analikosea Taifa na kujikosesha haki yake ya msingi yeye na vizazi vijavyo’’ amesema Andengenye.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa amewapongeza wanawake wanaotumia fursa za utekelezwaji miradi mbalimbali ya Maendeleo katika maeneo yao kwa lengo la kujipatia ajira za muda mfupi ili kujiongezea kipato na kumudu majukumu mbalimbali ya kimaisha.

Amesema wanawake hao wawe mfano wa kuigwa kwa wenzao katika Mkoa wa Kigoma na Tanzania kwa ujumla, kwa kuchangamkia fursa zinazojitokeza  ili kujipatia kipato halali kupitia shughuli mbalimbali za miradi ya maendeleo zinazotekelezwa na Serikali katika Maeneo yao.

Bi. Adelina Leonard, amesema utekelezaji wa miradi ya Serikali unawanufaisha kwa kupata ajira za muda ambazo zinawapatia kipato kwa ajili ya kujikimu kimaisha.

‘‘Kupitia miradi hii tunapata kazi ambazo zinatuweaesha kupata fedha za kununua mahitaji muhimu ya familia, lakini pia tunaposhirikiana na mafundi wazoefu nasisi tunapata ujuzi wa kiufundi ambapo tutaweza kwenda kufanya kazi sehemu nyingine mara mradi huu utakapokamilika’’ amesema Bi. Adelina.



Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa