• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

ONGEZENI KASI YA UKUSANYAJI MAPATO ILI KUWALETEA WANANCHI MAENDELEO-RC ANDENGENYE

Posted on: July 21st, 2023

Watendaji wa Serikali katika Halmashauri za Mkoa wa Kigoma wametakiwa kuongeza kasi katika kusimamia na kukusanya mapato ya ndani  ya Halmashauri kwa lengo la kuwaletea Maendeleo Wananchi.

Akizungumza kwenye kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kigoma, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye amesema kiwango cha Ukusanyaji wa mapato kitaongezeka kwa kutatua changamoto za uibuaji na usimamizi mzuri wa vyanzo vipya vya Mapato.

‘’Nijukumu letu viongozi wa Serikali katika Halmashauri zetu kuhakikisha utaratibu wa kukusanya Mapato ya ndani unazingatiwa kwa kufuata miongozo pamoja na kudhibiti viashairia vya upotevu wa makusanyo hayo’’ amesema.

Amewaeleza wajumbe kuwa, Halmashauri zinamapato ya kutosha lakini changamoto kubwa ni usimamizi wa vyanzo hivyo, wakusanya mapato pamoja na kutokufuatilia na kubaini ufanisi wa vitendea kazi.

Akiwasilisha taarifa ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023, Katibu Tawala Mkoa Kigoma Albert Msovela amesema Mkoa ulipokea kiasi cha Shilingi 197,461,488,206 kwa ajili ya kutekeleza Bajeti ya Maendeleo.

Amesema kutokana na fedha hizo, mkoa umefanikiwa kutekeleza  Miradi ya Ujenzi wa Nyumba, Ofisi za wakuu wa wilaya, kukarabati majengo mbalimbali ya Ofisi ikiwemo Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ambapo shughuli hizo zimegharimu Shilingi Bil 2.5.

Msovela amevitaja vipaumbele vya Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 kuwa ni uimarishaji wa Huduma za Jamii kwa Umma, kuendelea na ujenzi wa nyumba na Ofisi za watendaji wa Serikali, kuimarisha mifumo ya ukusanyaji wa mapato ya ndani pamoja na kufuatiliaji na kusimamia  Shughuli katika Sekta za Elimu, Uchumi na Uzalishaji.

Aidha Msovela amewashukuru na kuwapongeza viongozi wa Chama cha Mapinduzi kwa ufuatiliaji wao wa karibu katika Miradi mbalimbali inayotekelezwa na kutoa ushauri pale walipoona inafaa kufanya hivyo.

Pia Katibu Tawala amewashukuru watumishi wote wa Serikali kwa kazi nzuri wanazoendelea kuzifanya mkoani Kigoma katika kuhakikisha wanaihudumia Jamii pamoja na kusimamia vizuri miradi inayotekelezwa na Serikali.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa