• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

''MUHAS KIGOMA ITAIMARISHA HUDUMA BOBEZI ZA KITABIBU'' RC ANDENGENYE

Posted on: June 28th, 2023

Kuanzishwa kwa Kampasi ya  Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili Mkoani Kigoma kumeelezwa kuwa kutasogeza na kuongeza fursa za utolewaji wa huduma bobezi kutoka kwa  Madaktari bingwa pamoja na kuongeza  Ikama ya  watumishi katika Sekta ya Afya mkoani Kigoma.

Akizungumza kwenye kikao cha kupokea Taarifa ya Maendeleo ya Utekelezaji Mradi wa Ujenzi wa Kampasi hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye amesema pamoja na  mradi kujielekeza katika kupunguza changamoto za kimatibabu, utaongeza mnyororo wa Thamani na kuimarisha uchumi wa Mkoa wa Kigoma.

Amesema faida zitakazosababishwa na uwepo  wa Kampasi hiyo hazitokuwa upande wa Afya na Elimu pakee bali, kutakuwepo na fursa kwa wafanyabiashara wakubwa na wale wenye mitaji midogo kutoka ndani na nje ya Mkoa pamoja na nchi kuwekeza na kufanya Biashara zao mkoani hapa.

‘’Uwepo wa ongezeko la watu utakaosababishwa na ujio wa Chuo  hicho utapanua na kuimarisha Masoko yetu ya bidhaa zinazozalishwa na kupatikana ndani ya Mkoa wa Kigoma  kama Samaki, Dagaa, Mazao ya chakula na yale ya Biashara’’ amesema.

Kupitia Kikao hicho, Mkuu wa Mkoa amewaelekeza  wakuu wa Idara, Seksheni na Taasisi mbalimbali za Kiserikali kuhakikisha mahitaji yote ya muhimu yatakayowezesha ujenzi wa chuo hicho yanapatikana na na kufika eneo la ujenzi kwa wakati.

‘’Hatutarajii Taasisi za Serikali kukinzana katika kutekeleza zoezi la kufikisha Miundombinu muhimu kwa ajili ya ujenzi na ukamilishaji wa chuo. Shirikianeni na kuhakikisha  Maji, Umeme, mawasiliano na Barabara vinafika katika eneo husika bila kuwepo kwa sababu zozote za ucheleweshaji kwa kuogopa kuharibu miundombinu mingine’’ Amesisitiza Andengenye.

Akitoa Taarifa ya uanzishwaji wa mradi wa Kampasi hiyo, Mwakilishi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt.  Rehema Horera amesema mradi wa Ujenzi wa Kampasi ya MUHAS utatekelezwa na Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (Higher Education for Economic Tranformation)

Ameyataja Malengo ya Mahususi ya Mradi wa HEET kuwa ni  kuboresha miundombinu ya kufundishia na kujifunzia katika Taasisiza Elimu ya Juu, kuwaimarisha kitaaluma wahadhiri wa vyuo vikuu, kuboresha mifumo ya TEHAMA na Mitaala ya Elimu ya juu.

‘’Lengo lingine muhimu la Mradi huu ni kuboresha mitaala mia nne ya Elimu ya Juu nchini ili Mwanafunzi atakayemaliza Elimu ya Chuo Kikuu aweze kujiajiri au kuajirika kwa urahisi kutokana na kuwa na muelekeo toshelevu wa kiujuzi’’ amesema Dkt. Horera.

Naye Mratibu wa Mradi wa HEET-MUHAS Prof. Erasto Mbungi amesema Mradi huo utakapokamilika sambamba na Ujenzi wa Hospitali Kuu ya Kanda,  utapunguza Adha ya wananchi kwenda katika Hospitali kubwa zilizo nje ya Mkoa wa Kigoma kwa ajili ya kufuata huduma za matibabu za kibingwa.

Upande wake Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Dkt. Godfrey Smart ameishukuru Serikali kwa kuuelekeza Mradi huo mkoani Kigoma kwani utaongeza idadi ya wataalam pamoja na kuimarisha matibabu ya kisasa.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa