• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

MSOVELA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA WATUMISHI WA UMMA

Posted on: October 6th, 2023

KATIBU TAWALA WA MKOA WA KIGOMA ALBERT MSOVELA AKIZUNGUMZA NA WATUMISHI WA UMMA KATIKA HALMASHAURI YA MJI WA KASULU(HAWAPO PICHANI) IKIWA NI MUENDELEZO WA ZIARA YAKE YA KUZUNGUMZA NA WATUMISHI WA UMMA KATIKA HALMASHAURI NANE ZA MKOA WA KIGOMA.

Watumishi wa Umma mkoani Kigoma wametakiwa kuimarisha ushirikiano katika maeneo ya kazi ili kuongeza ufanisi katika utendaji kazi na kuharakisha utatuzi wa changamoto zinazowakabili wananchi katika Jamii.

Akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Mji Kasulu, Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma Albert Msovela amesema ni muhimu kwa watumishi kuwa na Ushirikiano ili kuchochea uboreshaji wa utoaji wa Huduma kwa Wananchi.

Amesema baadhi ya watumishi wa Umma hutumia muda mwingi kuvutana na kusengenyana hali inayochochea migogoro katika maeneo ya kazi badala ya kutekeleza majukumu yao ya kiutumishi huku  wakisababisha wananchi kukosa huduma za kuridhisha.

‘’Kama hakuna umoja, mshikamano, kuheshimiana na  kuzingatia mtitiriko wa mipango kazi inayowekwa na Serikali, hatuwezi  yetu na matokeo chanya ya mipango hiyo hayataweza kupatikana’’ amesema.

Ninaamini pamoja na uwepo wa Sheria na taratibu za kiutumishi, kama hakuna upendo miongoni mwetu, nidhamu ya kazi, kujitolea na kujituma, daima itakuwa vigumu kuleta tija katika utendaji wetu.

‘’Nasisitiza mfanye vikao vya mara kwa mara vitakavyohusisha Idara na vitengo, vikao vya kisheria vya Halmashauri, mkutane na wadau wenu wa Maendeleo pamoja na kushirikishana katika maamuzi mbalimbali pamoja na usimamizi wa miradi inayotekelezwa katika Halmashauri’’ amesisitiza.

Aidha Katibu Tawala huyo amewaasa watumishi  hao kuongeza nguvu katika usimamizi wa mapato ya ndani ili kuiwezesha Halmashauri kujiendesha.

‘’Ukusanyaji wa mapato kwa kutumia mfumo wa Tausi iwe Agenda ya msingi kila mtakapokutana ili kuimarisha makusanyo ya ndani’’ alisisitiza Msovela.

Naye Mhasibu Mkuu wa Mkoa Johnson Gamba amewasisitiza watumishi hao kujenga nidhamu ya matumizi ya Fedha huku wakizingatia Kanuni na Taratibu zinazoongoza matumizi ya Fedha za Umma.

Aidha kupitia wasilisho lake kwa watumishi hao, Gamba amemwelekeza Mkurugenzi na Mweka Hazina kutekeleza majukumu yanayohusu matumizi ya fedha kwa kuzingatia uwazi na ushirikishwaji wa watumishi wanaohusika na matumizi hayo.

Upande wake Zainab Mkamba ambaye ni Afisa Utumishi na Rasilimali watu Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kigoma, ametoa wito kwa watumishi hao kuzingatia maadili na taratibu za kiutumishi.

‘’Tunahudumia jamii hivyo tuzingatie tabia na mienendo inayozingatia miongozo ya kiutumishi ili tuweze kuwa mfano kwa jamii’’ amesisitiza Zabibu.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa