• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

MSOVELA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KATIKA MASUALA YA AFYA

Posted on: September 9th, 2023

KATIBU TAWALA  MKOA WA KIGOMA ALBERT MSOVELA AKIZUNGUMZA NA WASHIRIKI WA KIKAO CHA  KAMATI YA MSINGI YA  AFYA MKOA WAKIGOMA (HAWAPO PICHANI) KILICHOFANYIKA KATIKA UKUMBI WA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA SEPTEMBA 8, 2023. KUSHOTO KWAKE NI MGANGA  MKUU WA MKOA WA KIGOMA DKT. JESCA LEBBA.

WASHIRIKI WA KIKAO CHA KAMATI YA  MSINGI YA AFYA MKOA WA KIGOMA WAKIFUATILIA JAMBO WAKATI WA KIKAO.

Jamii mkoani Kigoma imetakiwa kuchukua tahadhari na kujikinga dhidi ya magonjwa kwa kuzingatia kanuni za Afya pamoja na kushirikiana na Serikali kupitia wataalam wa Afya ili kupambana na kudhibiti maradhi mbalimbali yanayojitokeza katika maeneo yao.

Wito huo umetolewa na Katibu Tawala Mkoa  Kigoma Albert Msovela alipofungua mafunzo kwa Kamati ya Msingi ya Afya Mkoa, yaliyolenga kuijengea uwezo katika kutoa Elimu kwa Jamii kuhusu Kampeni ya utoaji chanjo ya Polio inayotarajia kuanza kutekelezwa mkoani hapa Septemba 21 hadi 24, 2023.

Amesema Serikali kupitia Wizara ya Afya imebaini na kuthibitisha uwepo wa ugonjwa wa Polio katika baadhi ya maeneo nchini pamoja na nchi jirani, hali iliyosababisha ichukue hatua za makusudi kwa lengo la kukabiliana na ugonjwa huo.

Amesema tayari serikali imetoa chanjo 1,105,000 kwa ajili ya kuchanja na kutoa kinga kwa watoto wote walio na umri chini ya miaka nane kwa mkoa wa Kigoma, ambapo zoezi hilo litafanyika nyumba kwa nyumba, kupitia vituo vya kutolea Huduma za Afya, Shuleni pamoja na maeneo mengine yenye mikusanyiko ya watu.

Amesisitiza kuwa, ili kufanikisha malengo ya kampeni hiyo,  kila Mwananchi anapaswa kushiriki kuwasaidiia watoa huduma katika kuwabaini walengwa wote ili waweze kufikiwa na kupatiwa chanjo hiyo.

Aidha Msovela ametoa Rai kwa wakazi mkoani hapa kuendelea kuzingatia kanuni za Usafi ikiwemo kunywa maji safi na salama pamoja na kutumia vitakasa mikono kwa lengo la kuepuka na kudhibiti uwezekano wa kuibuka na kuenea kwa maradhi ya tumbo.

Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Dkt. Jesca Lebba amesema wataalam wa Afya wanaendelea kukabiliana na kuchukua hatua za kitabibu dhidi ya wahisiwa wa maradhi ya Surua  pamoja na waliobainika kuwa na maradhi ya kuhara katika wilaya ya Kibondo mkoani hapa.

Aidha amesisitiza kuwa, kutokana na muingiliano wa Raia kutoka nchi jirani, wakazi wenyeji wanatakiwa kuchukua tahadhari na kutoa taarifa mapema wanapobaini dalili za uwepo wa Maradhi mbalimbali katika maeneo yao.

Akiwasilisha mada kwa Kamati hiyo, Mratibu wa chanjo Mkoa wa Kigoma Yohanes Mwitanyi amezitaja njia za kujikinga na maradhi ya Polio ikiwa ni pamoja na kutakasa mikono nyakati zote, kutumia vyoo,  kunywa maji safi na salama, kula chakula kilichoandaliwa kwa usafi pamoja na kuosha vyakula kabla ya kula.Mratibu huyo wa chanjo amewataka washiriki wa kikao hicho kuwa mabalozi wazuri wa chanjo ya Polio kwa kuuelimisha Umma kuhusu Usalama wa chanjo hiyo na umuhimu wake ili kumuepusha mtoto dhidi ya ulemavu unaosababishwa na kupooza ghafla kwa viungo vya mwili.

‘’Niwaombe kwa nafasi zenu, ukiwa kiongozi wa dini, mwakilishi wa mashirika binafsi, kiongozi katika taasisi za Umma, wataalam pamoja na wanahabari, sote tutumie majukwaa tunayoyafikia kufikisha ujumbe huu muhimu kwa jamii ili iweze kujenga utayari na muitikio chanya kuhusiana na zoezi hili ili liweze kufanikiwa kwa asilimia mia mkoani kwetu’’ amesisitiza Mwitanyi.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa