• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

MRADI WA SHULE BORA KUENDELEA KUIMARISHA MIFUMO YA KIELIMU KIGOMA

Posted on: March 6th, 2024

Watendaji wa Serikali katika ngazi za Halmashauri mkoani Kigoma wameshauriwa kuimarisha ushirikishwaji wa wananchi kabla na wakati  wa kutekeleza miradi ya maendeleo inayotokana na fedha kutoka kwa wafadhili ili kuifanya miradi hiyo kuwa endelevu.

Ushauri huo umetolewa na Dkt. John Lusingu Mshauri wa masuala ya kielimu katika ubalozi wa Uingereza nchini, alipozungumza akiwa katika ziara ya kukagua na kufanya Tathimini ya utekelezaji wa miradi ya Maendeleo inayotekelezwa chini ya programu ya Shule Bora wilayani Buhigwe mkoani hapa.

Amesema watendaji katika ngazi za halmashauri hususani Mkurugenzi kwa kushirikiana na wataalam kutoka Idara ya Elimu, wanapaswa kukaa na kuwahusisha wananchi hatua zote za utekelezaji wa miradi hiyo kwani  hupelekewa katika maeneo yao ikiwa na mipango kazi ambayo watekelezaji wakuu ni wananchi.

Amefafanua kuwa, Miradi yote huja na mipango kazi hivyo walengwa wanapokuwa na uelewa kuanzia kwenye mipango kazi hadi utekelezaji wake, huifanya miradi hiyo iweze kudumu kutokana na wao wenyewe kumudu kuiendesha, jambo litakalosaidia iweze kuwanufaisha kwa muda mrefu kama ilivyokusudiwa.

Kupitia ziara hiyo, Dkt. Lusingu amesema ameshuhudia mapinduzi na mafanikio makubwa ya utekelezaji wa mradi wa Shule Bora wilayani Buhigwe ambapo shule zinazotekeleza mradi huo zimeweza kuibua shughuli za uzalishaji mali ikiwemo  upandaji wa misitu na baadhi ya shule hizo zikiwa zimefanikiwa kuivuna misitu hiyo na kutumia fedha zilizopatikana kwa ajili ya kuanzisha miradi mingine ikiwemo ujenzi wa nyumba za walimu.

Ameyataja mafanikio mengine yaliyofikiwa wilayani Buhigwe kuwa ni uanzishwaji wa kilimo cha  zao la Kahawa, Ufugaji wa nyuki, kuku, sambamba na miradi mbalimbali  na kuwa vyanzo vya mapato katika shule hizo.

Mwalimu Judith Ndiga wa Shule ya Msingi Mkatanga, amesema utekelezaji wa Mradi wa Shule Bora kupitia Programu ya UWAWA, umefanikiwa kuanzisha utaratibu wa kudumu kwa ajili ya kutoa chakula kwa wananfunzi shuleni hapo, jambo linalosaidia katika kuongeza ufanisi wa kitaaluma na kupunguza utoro.

‘‘Utaratibu huu wa kuwapatia wanafunzi wetu chakula hapa shuleni umesababisha waweze kujenga tabia ya kufika shuleni bila msukumo wowote wa wazazi  au walimu, aidha utaboresha kiwango cha ufaulu sambamba na kuimarisha Afya za watoto’’ amesisitiza Mwalimu Judith.

Upande wake Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mnyegera iliyopo wilayani Buhigwe Fidel Ernest amesema mara baada ya kuanza utekelezaji wa programu  ya mafunzo  endelevu ya walimu kazini(MEWAKA) hali ya kujiamini kwa walimu kiufundishaji imeongezeka sambamba na ongezeko la ufaulu hadi kufikia zaidi ya Asilimia 90 kwa Mwaka 2023.

Aidha Mwalimu Ernest amesisitiza kuwa maboresho makubwa yay a miundombinu ya kielimu yanayofanywa na serikali kupitia mradi huo, yameendelea kuyafanya mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji kuwa rafiki kwa walimu pamoja na wanafunzi hali inayoendelea kuimarisha utoaji wa elimu yenye ubora kwa watoto.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa