• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

MRADI WA HEWA UKAA FURSA MPYA YA KIUCHUMI MKOANI KIGOMA

Posted on: January 26th, 2024

Shughuli mbalimbali za kibinadamu zinaelezwa kuwa ndicho chanzo kikubwa cha mabadiliko ya Tabianchi huku zikisababisha uzalishwaji mkubwa wa Hewa Ukaa ambayo huathiri mwenendo wa hali ya hewa na kusababisha mafuriko, ukame, joto kali, baridi iliyopitiliza, vimbunga na hata kuhatarisha usalama wa maisha ya viumbe hai.

Namna bora ya kukabiliana na mabadiliko hayo ni kudhibiti uharibifu wa misitu ya Asili iliyopo na kuongeza kasi katika upandaji wa misitu mipya na kuitunza, kwani uwepo wake umethibitishwa na wataalam wa Mazingira kufyonza hewa ukaa inayosababishwa na kazi mbalimbali za uzalishaji zinazopelekea uchafuzi wa mazingira.

Mpango wa udhibiti wa Hewa ukaa kupitia misitu sambamba na kuongeza ufanisi katika mchakato wa utunzaji wa Mazingira,  kwa Mujibu wa Chapisho la Gazeti la Habari Leo Feb 15, 2021, hii ni biashara iliyothibitisha kuwainua kiuchumi wakazi wa Katavi kwa kufanikiwa kuuza Tani 82,000 za Hewa hiyo kwa Thamani ya Shilingi 250,000,000. 

Kupitia chapisho hilo, Fedha zinazopatikana sambamba na kuwanufaisha wananchi zimekuwa zikitumika katika kutekeleza miradi ya maendeleo kama ujenzi wa miundombinu ya kielimu, Afya na kusogeza nishati ya Umeme. 

Serikali ya Mkoa wa Kigoma imefanikiwa kutia saini katika utekelezaji wa Awali wa Mkataba wa kuanza kwa mradi huo utakaosimamiwa na kuratibiwa na Kampinu ya Ørsted Nature Based Solution A/S kwa kushirikiana na Shirika la Kuhudumia wakimbizi la Denmark (DRC). 

Biashara hii itaanza kufanyika katika Halmashauri za Wilaya Kakonko, Kibondo na Kasulu ambapo kwa sasa utambuzi na upembuzi yakinifu uliolenga kubaini maeneo hitajika umeshafanyika na hatua iliyobaki ni kukutana na wananchi kwa ajili ya kuwapa elimu, kuridhia utoaji wa maeneo ya vijiji hususani yale yanayomilikiwa na Serikali pamoja na kuingia mikataba rasmi kwa ajili ya kuanza kwa zoezi hilo. 

Maisha ni kupanga na kuchagua, jukumu la wananchi hususani katika maeneo yaliyotambuliwa ni kuhakikisha wanaunga mkono mpango huu bila kuingiza mivutano isiyo na tija kwa mustakabali wa maendeleo yao binafsi pamoja na Halmashauri walizopo. Ifahamike kuwa zoezi la uanzishaji wa Mradi huu ni shirikishi na uhalali wa utekelezaji wake utategemea ridhaa ya wananchi. 

Sambamba na manufaa kiuzalishaji, shughuli za kibinadamu kupitia viwanda husababisha athari kubwa ya za kimazingira kupitia hewa hiyo na madhara yake tunaendelea kuyashuhudia kila uchao hivyo hatuna budi kuunga mkono juhudi za serikali kwa kushirikiana na wadau ili sote tuweze kutunza mazingira ambayo ni urithi wetu wa Asili kwa lengo la kujipatia mkate wa kila siku kupitia mauzo ya hewa hiyo ambapo hatutolazimika kibarua cha kututoa jasho kufikia uzalishaji.

Ni jukumu la kila mkazi hususani katika maeneo yatakayopata fursa ya kuguswa na mradi huo kuitumia fursa  hiyo sambamba na kutunza mazingira bali kujikusanyia ukwasi kwa ajili ya kumudu gharama za maisha na kuleta maana halisi ya lengo la serikali katika kumuinua mwananchi kiuchumi.

Rai yangu kwa wakazi ni kushiriki vikao vya maamuzi vitakavyowakutanisha na wataala wa mradi katika maeneo yao ili waweze kujengewa uelewa wa kina kuhusu hatua za utekelezaji na faida za mradi badala ya kusubiri tetesi kutoka kwa wapinga maendeleo  kupitia porojo za vinywa vyao.

 


 


Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa