• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

MPANGO AIPONGEZA NMB UFADHILI MIRADI YA MAWNDELEO

Posted on: July 4th, 2023


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango ameupongeza Uongozi wa Benki ya NMB Nchini kwa kuendelea kutoa Fedha kwa ajili ya Ufadhili wa Miradi mbalimbali ya Maendeleo pamoja kuendesha Program ya uhifadhi wa Mazingira.

Makamu wa Rais ametoa pongezi hizo alipozungumzana Wananchi wa Wilaya hiyo  baada ya kuzindua  Tawi  Jipya la Benki ya NMB katika Wilaya ya Buhigwe Mkoani hapa.

Amesema Benki hiyo imekuwa ikitoa Fedha nyingi kupitia gawio, ambazo kimsingi zimeendelea kutumika katika kutekeleza miradi mbalimbali nchini kwa lengo la kuwaletea Maendeleo wananchi.

Amesema serikali imekuwa ikitumia Fedha hizo katika kutekeleza miradi mbalimbali ya Huduma za Jamii kama vile Maji, Umeme, Elimu, Barabara pamoja na Afya.

Dkt. Mpango ameendelea kufafanua kuwa, Benki ya NMB imeendelea kutumia fedha nyingi katika kufadhili mradi wa upandaji wa miti katika Maeneo mbalimbali nchini kwa lengo la kutunza Mazingira.

Kuhusu umuhimu wa kufunguliwa kwa Huduma hiyo ya kifedha wilayani Buhigwe, Dkt. Mpango amesema ‘’itawapunguzia kero ya kufuata huduma za kibenki mbali na maeneo yao ya makazi pamoja na kuwatoa wananchi kwenye mfumo usio rasmi wa kuhifadhi Fedha zao’’

‘’Baadhi ya wananchi walilazimika kufuata Huduma hii kwa umbali wa Km. 70, jambo ambalo lilisababisha baadhi ya wananchi kutunza Fedha  kupitia mifugo, mashamba na hata kuzitunza ndani kwa kutumia utaratibu usio sahihi’’

‘’Niwasisitize viongozi wa NMB mhakikishe Benki hii inatoa fursa ya upatikanaji wa mikopo kwa wajasiriamali wadogo, vikundi vya  wanawake pamoja na  wakulima wadogo ili waweze kujiimarisha kiuchumi’’ ameendelea kusisitiza.

Aidha Dkt. Mpango amezielekeza Benki mbalimbali nchinikufanya utafiti ili kubainimaeneo yanayokidhi kuanzishwa huduma na kufungua matawi ya Benki hizo, mawakala na mifumo mingine itakayorahisisha utoaji na upatikanaji wa Huduma za kifedha.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Thobias Andengenye amewaasa wakazi wa Wilaya ya Buhigwe kunza kutumia fursa zote za Huduma za kifedha zitakazotolewa na Benki hiyo kwa lengo la kujiletea Maendeleo.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Thobias Andengenye amewaasa wakazi wa Wilaya ya Buhigwe kunza kutumia fursa zote za Huduma za kifedha zitakazotolewa na Benki hiyo kwa lengo la kujiletea Maendeleo.

‘’Huduma za kibenki zitolewazo na Taasisi hii ya kifedha ni za uhakika na zimeendelea kugusa makundi yote  yenye lengo la kupata huduma za mikopo midogo’’  amesema.

Philbert Mponzi ambaye ni Kaimu  Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB Tanzania, amesema tawi la Benki hiyo lililozinduliwa Buhigwe ni la 229, huku Taasisi hiyo ikifanikiwa kuanzisha Mashine za ATM 780 pamoja na kuwezesha asilimia 95 ya miamala ya Fedha kufanyika nje ya Benki kwa lengo la kuongeza fursa za ajira kwa wananchi.

Mponzi amesema kuwa Taasisi yao itatoa Elimu ya masuala ya kifedha na kuibua ubunifu kwa lengo la kuwajengea uwezo wananchi katika kujiongezea kipato na kuimarisha uchumi wao binafsi na mkoa kwa ujumla.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa