• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

MNYETI AAGIZA UDHIBITI ZANA HARAMU ZA UVUVI

Posted on: November 18th, 2023

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Alexander Mnyeti amewataka maafisa Uvuvi mkoania Kigoma kuongeza kasi katika kudhibiti kuenea kwa zana haramu za uvuvi kabla ya kuwafikia wananchi ili kuwaepushia hasara kutokana  na hizo kukamatwana kuteketezwa na serikali.

Mnyeti ametoa kauli hiyo alipozungumza kwenye hafla ya kukabidhi boti tisa za Uvuvi kwa wanufaika mkoani Kigoma huku akisisitiza kuwa lengo la Serikali ni kuimarisha uchumi wa wananchi kwa kuhamasisha na kuongeza tija katika uzalishaji kupitia mazao ya Samaki.

Naibu waziri huyo amewaelekeza maafisa uvuvi kufuatilia na kuhakikisha wanafunga maduka na kuwakamata wafanyabiashara wote wanaouza nyavu ambazo kisheria haziruhusiwi kutumika kwa shughuli za uvuvi nchini.

‘’Nendeni mkafanye msako katika maeneo yote yanayozalisha, kuuza na kufanya matumizi ya zana haramu za uvuvi na kuzidhibiti ili zisitumike katika mito, mabwawa, maziwa na bahari zetu’’ ameagiza Mnyeti.

Naibu waziri huyo amewakumbusha watendaji hao wa serikali kutekeleza wajibu wao wa kutoa Elimu na miongozo ya uvuvi bora badala ya kusubiri wavuvi wafanye makosa kisha kuwatoza fedha kutokana na makosa hayo, hali inayosababisha baadhi yao kufilisika.

‘’Baadhi yenu mmegeuka wakusanya mapato wa Halmashauri badala ya kusimamia majukumu yenu ya msingi ya kutoa elimu na kusimamia taratibu za uvuvi’’ amesisitiza  Mnyeti.

Baadhi ya wanufaika wa zana hizo za uvuvi zilizotolewa kwa njia ya mikopo nafuu kutoka serikalini wamesema wanauhakika wa kurejesha mikopo yao kutokana na vyombo  hivyo kutumia mifumo ya kisasa katika mchakato wa uvuvi.

Amesema ziwa Tanganyika linasamaki wengi lakini changamoto iliyokuwa ikiwakabili ni kukosa zana za kisasa kwa ajili ya kutekeleza majukumu  yao ya uvuvi.

Jumla ya boti Tisa zenye Thamani ya Shilingi Mil.535 zimekabidhiwa kwa vikundi vya wanufaika katika Halmashauri ya Kigoma, Uvinza na Manispaa ya Kigoma Ujiji.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa