• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

MKOA WA KIGOMA KUWA KINARA WA KILIMO CHA ZAO LA CHIKICHI

Posted on: December 1st, 2017


Mkoa wa kigoma umenuia kuwa kinara wa kilimo cha zao la chikichi na kuzalisha bidhaa mbalimba zitokanazo na zao hilo kwa kuanzisha mpango kazi kabambe na mikakati ya kilimo cha chikichi.

Uongozi wa Mkoa wa Kigoma umeandaa mpango wa kuendeleza zao la chikichi unaozingatia kunua zao hili ili liwe sehemu kubwa ya bidhaa ghafi katika kufanikisha adhma ya viwanda vya Mkoa kuanzisha kiwanda cha kuchakata mawese.

Takwimu zinaonesha kuwa mwaka wa 2000 hadi 2007 zaidi ya 95% ya mafuta ya kula yaliyoagizwa nchini yalikuwa ni mawese. Pia takwimu zinaonesha kuwa kwa mwaka wa 2016, mahitaji ya Taifa ya mwezi ya mawese yalikuwa ni tani 50,000, wakati uzalishaji wa mafuta haya kwa mwaka ni tani 40,000 zikiwemo tani 30,000 zinazozalishwa na Mkoa wa Kigoma

Kutokana na takwimu hizi ni dhahiri kuwa uzalishaji wa mafuta ya mawese haukidhi mahitaji ya Taifa ambayo ni tani 600,000 kwa mwaka ikiwa ni upungufu wa tani 560,000.

Uagizaji wa mafuta ya mawese umeongezeka kutoka tani 3,000 mwaka wa 1978 hadi tani 510,000 mwaka jana 2016 na utaongezeka kwa miaka ijayo.

Aidha utumiaji wa fedha za kigeni kuagiza mawese kutoka nje umeongezeka kutoka dola za kimarekani 13,000,000 mwaka 1961 hadi zaidi ya 320,000,000 kwa mwaka wa 2016.

Kigoma ni Mkoa pekee unaolima zao la michikichi kwa wingi nchini Tanzania ukiwa na hekta 18,924 zenye michikichi inayozalisha tani 30,010 ambayo ni tani 1.6 kwa hekta za matunda ya chikichi. Uwezekano wa uzalishaji ni tani 75,700 sawa na tani 4.0 kwa hekta kwa eneo lililopo lenye michikichi.

Hali ya uzalishaji wa chikichi Kigoma kwa sasa inaonekana kuwa bado ipo chini kwa sababu uzee wa michikichi iliyopo, mashamba kutokutunzwa kitaalam, ukosefu wa mbegu bora pamoja na teknolojia duni ya uchakataji wa zao hilo.

Mpango wa Mkoa unalenga kuwa na viwanda 7 vya kisasa vya kusindika malighafi itakayozalishwa, Kiwanda kikuu kimoja kitakachoweza kusindika mawese ghafi, Viwanda vidogo vinne vitawekwa kwenye vijiji vitakavyopendekezwa na MSM, Kiwanda kimoja kwa ajili ya usindikaji wa mafuta ya alizeti. Baada ya miaka kadhaa, Mkoa unatarajia kujenga kiwanda cha kutengeneza gesi kutokana na mashudu ya michikichi.

Ili kuongeza tija ya zao la chikichi Mkoa unahamasisha wilaya zote zenye maeneo yanayofaa kwa kilimo cha chikichi, kufufua mashamba na kuanzisha mapya. Pamoja na kuvutia makampuni binafsi kuzalisha miche bora na kuisambaza kwa wakulima.

Mpango wa kuinua zao la chikichi Kigoma umepanga kuanza na wakulima 100,000 ambao watapewa mbegu

zilizoboreshwa (chotara) kila mmoja miche 150 ambayo itatosha kupanda eneo la hekta moja ekari mbili na nusu.

Kwa sasa mbegu bora hazipatikani nchini kwetu bali zinaagizwa kutoka nchi kama Costa Rica, Malaysia na Indonesia kwa gharama ya dola ya kimarekani moja kwa mbegu moja.

Njia mbadala ambayo Mkoa umepanga ni kuwa na kituo chake cha uzalishaji mbegu na maabara. Hiki kituo kitafanya utafiti na uzalishaji wa miche bora kwa kutumia mfumo wa kisasa ili kuzalisha miche mingi kwa gharama ndogo na kwa  muda mfupi.

Uongozi wa Mkoa wa Kigoma unaona kuna umuhimu wa zao la chikichi kuwa na bodi ya zao la chikichi ili kusaidia uendelezaji wa kilimo cha zao hilo. Aidha, wananchi wabadilishwe mtazamo juu uendelezaji wa zao la chikichi. Wananchi wahamasishwe ili wajiunge na walime kupitia vyama vya ushirika.


Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa