• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

Mkuu wa Mkoa akerwa na Waratibu wa Malaria

Posted on: July 23rd, 2019

Mkuu waa Mkoa wa Kigoma Brig. Gen. Emmanuel Maganga amesema haridhishwi na utendaji kazi wa maafisa wanaoshughulikia Malarai Mkoani Kioma na kwamba wajitathmini kabla ya kuanza kuchukuliwa hatua za kushindwa kusimamia majukumu yao, kwani badala ya kushuka kwa takwimu za maambukizi ya malaria Mkoani Kigoma, badala yake kunaongezeko la maambukizi ya ugonjwa huo.


Mkuu wa Mkoa amesema haya wakati akizundua kampeni ya ugawaji wa vyandarua kupitia shule shule za msingi, amesema takwimu za sasa zinaashiria ukubwa wa tatizo la malaria katika mkoa kuwa juu, ukilinganisha na mikoa mingine. Hali hii inajidhirisha katika takwimu za Viashiria vya Ugonjwa wa malaria kwa Watoto chini ya miaka 5 ya mwaka 2017 ambapo kigoma ilionekana kuwa na asilimia 24.4, kiwango cha juu kuliko mikoa yote Nchini huku wastani wa Kitaifa ikiwa ni asilimia 7.3%



Amesema kasi ya mapambano ya malaria kwa Mkoa wa Kigoma inaonekana ipo chini na hivyo kutishia kutofikia kwa Malengo ya kutokomeza ugonjwa huo. Kutokana na hali hii amewaambia Maafisa wanaohusika na program ya utokomezaji wa Malaria kwa kila Wilaya kujitathmini na kibidi waachie nafasi hizo kabla ya kuchukuliwa hatua. Natoa agizo kwa viongozi wote kuanzia ngazi ya Mkoa na Halmashauri kuhakikisha afua za kupambana na Malaria zinakuwa ni ajenda ya vikao vyote vya maamuzi na utekezaji wa afua hizi upimwe kila mwezi kuanzia leo hii ameongeza Mkuu wa Mkoa.


Awali akitoa taarifa Mganga Mkuu wa mkoa wa Kigoma Dkt. Paul Chaote amesema takwimu kutoka vituo vya kutolea huduma za afya mwaka 2017 Mkoani Kigoma zinaonesha kuwa asilimia 33.5 ya wagonjwa waliohudhuria kupata huduma za nje (OPD) walikutwa na ugonjwa wa malaria na mwaka 2018, asilimia 29.2.  Vivyo hivyo katika mwaka 2019, hadi mwezi wa 6, asilimia 28.98 ukilinganisha na magonjwa mengine.


Malengo ya mapambano dhidi ya malaria nchini Tanzania ni kupunguza kiwango cha malaria kufikia chini ya asilimia 1 ifikapo mwaka 2020 na  hatimaye kutokomeza malaria ifikapo 2030.


Tayari hatua za kupambana na ugonjwa huo mbaya zimeanza kwa kuzindua kampeni ya ugawaji vyandarua ya Ugawaji wa vyandarua kwa wajawazito, Watoto wa miezi 9 kupitia vituo vya kutolea huduma za afya na Kupitia wanafunzi wa shule ya Msingi na zoezi la unyunyiziaji wa viuadudu kwenye mazalia ya mbu.


Imeelezwa kuwa hadi sasa Mkoa  wa Kigoma umepokea kiasi cha lita 7616 za viududu vya  kibaiologia kutoka Wizara ya Afya kupitia Mpango wa Taifa wa kudhibiti Malaria na Ofisi ya Rais TAMISEMI ambayo tayari vimesambazwa katika Halmashauri zote 8 za mkoa wa Kigoma ambapo Jumla ya Majengo 248,000 yanatarajiwa kupuliziwa


Maandalizi ya Upuliziaji wa Kiuatilifu Cha Ukoko Majumbani yameanza ambapo mwaka huu zoezi hili litafanyika katika halmashauri za wilaya za Kakonko, Kibondo na Kasulu, pamoja na kuhusisha kambi za wakimbizi zote tatu. Lengo la zoezi hili ni kupunguza kiwango cha malaria kwa kiasi kikubwa na kupunguza vifo vya mama wajawazito na watoto chini ya miaka mitano.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa