• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

MICHE MIL.4.5 KUGAWIWA BURE KWA WAKULIMA WA KAHAWA MKOANI KIGOMA

Posted on: August 21st, 2023

Katika kuhakikisha Kilimo kinaendelea kuwa Muhimili muhimu wa kiuchumi mkoani Kigoma, Bodi ya Kahawa nchini kwa kushirikiana na Taasisi ya Utafiti wa Kahawa (TaCRI) wanatarajia kuzalisha miche ya mbegu bora ya Kahawa Mil. 4.5 na kuigawa bure kwa wakulima wa zao hilo mkoani hapa katika msimu wa Kilimo wa Mwaka 2023/2024.

Hayo yamebainishwa na Afisa Ugani na Msimamizi wa Mradi wa Kitalu cha Miche bora ya Kahawa kilichopo kata ya Kalinzi wilayani Kigoma, Richard Nelson alipotoa taarifa ya utekelezaji kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2023 alipotembelea na kukagua mradi huo.

Ameeleza kuwa, hadi kufikia mwaka 2026 kilimo cha zao hilo kitaongezeka maradufu mkoani Kigoma kutoka Hekta 1500 zinazolimwa sasa na kufikia Hekta 3000 kutokana na kuongezeka kwa eneo la uzalishaji, kutakakosababishwa na ongezeko la upatikanaji wa miche ya bure.

Amesisitiza kuwa sambamba na wananchi kutarajiwa kunufaika kiuchumi kutokana na ongezeko la uzalishaji, Kilimo cha zao hilo kitaongeza makusanyo ya ndani ya Halmashauri ya Kigoma na kuimarisha uwezo pamoja na fursa ya utekelezaji wa miradi ya Maendeleo.

Miche hiyo inatarajia kuwa mkombozi kwa mkulima kutokana na kuwa na ongezeko la Tija katika uzalishaji ikilinganishwa na iliyopo  sasa ikiwa na uwezo wa Tani 1 huku mbegu mpya ikizalisha tani 1.5 kwa Mwaka.

Mradi huo wenye Thamani ya Shilingi Mil. 750, unatarajia kuanza kugawa miche hiyo kwa wakulima wa Kahawa wilayani humo kuanzia mwanzoni mwa Mwezi Januari 2024.

Aidha mbio za Mwenge wa Uhuru zimehitimishwa wilayani humo baada ya kukagua, kutembelea, kuweka Mawe ya Msingi kwenye Jumla ya Miradi mitano ikiwemo Barabara ya Lami yenye urefu wa Km. 0.5, Ujenzi wa Madarasa Manne pamoja na vyoo katika Shule ya Msingi Kidahwe, Kituo cha Afya Kalinzi, Kitalu cha Miche ya Kahawa kalinzi pamoja na kikundi cha wanawake ‘’Mwakeye’’ kilichopo kijiji cha Mkigo ikiwa na Thamani ya zaidi ya Shilingi Bil.1.9.

Pia mbio hizo zimezindua klabu ya kupinga Rushwa Shule ya Sekondari Bitale, Mradi wa Uhifadhi wa Mazingira Shule ya Sekondari Mikamba pamoja na uzinduzi wa klabu ya Mazingira Shule ya Msingi Kidahwe na kupokea miradi yote katika Halmashauri hiyo.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa