• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

MHE. DKT. MPANGO AANZA ZIARA YA KIKAZI MKOANI KIGOMA

Posted on: July 8th, 2024


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango ameuelekeza uongozi wa Serikali mkoani hapa kuwachukulia hatua watumishi watakaobainika kushiriki kuruhusu uingizaji wa mifugo wilayani Uvinza kinyume cha Sheria na kusababisha ongezeko la migogoro baina ya wakulima na wafugaji.


Dkt. Mpango ametoa kauli hiyo alipozungumza kwa nyakati tofauti na wakazi wa wilaya ya Uvinza akiwa katika ziara yake ya kikazi mkoani hapa ambapo amesema baadhi ya watumishi wa Umma wasio waadilifu wamekuwa wakipokea fedha kinyume na sharia ili kuwaruhusu wafugaji kuingiza mifugo wilayani humo bila kufuata taratibu zilizowekwa na serikali.

‘‘Mamlaka za vijiji zinapaswa kuzingatia Sheria na Kanuni za matumizi bora ya Ardhi pia nakuagiza Mkuu wa Mkoa pamoja na watendaji wako kuchukua hatua dhidi ya wale wote wanaohusika na zoezi hilo bola kuzingatia maelekezo ya serikali kuhusu taratibu za ufugaji kwani nchi haitegemei mifugo pekee’’ amesema Dkt. Mpango.

Sambamba na hayo kupitia ziara yake makamu wa Rais amekagua ujenzi wa barabara ya Malagarasi, Ilunde hadi Uvinza yenye urefu wa Km. 51.1ambayo ujenzi wake umefikia Asilimia 54 huku ikitarajiwa kukamilika Machi, 2025.

Mara baada ya kukagua mradi huo, Makamu wa Rais amemshauri Mkandarasi anayetekeleza mradi huo kuhakikisha anatumia kipindi hiki cha kiangazi kukamilisha maeneo muhimu ya ujenzi wa barabara hiyo bila kuathiri ubora wa kazi.

Amesema lazima barabara zikamilike kwa wakati ili kutimiza malengo ya  Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu ya kutaka kuufungua mkoa wa Kigoma ili uweze kuwa Kitovu cha Biashara na Uchumi kwa ukanda wa Magharibi.

Aidha Dkt. Mpango amekagua na kuonesha kuridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa vituo vya kupoza umeme mkondo wa KV 132 kilichopo wilayani Uvinza  Kata ya Nguruka wilayani Uvinza pamoja na kituo kama hico cha MV A60 kilichopo kidahwe Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma.

Aidha Mhe. Makamu wa Rais amepata fursa ya kuzungumza na wakazi wa kijiji cha Kazuramimba na kusisitiza kuwa, serikali itaendelea kuhakikisha inasogeza huduma za jamii jirani na wananchi sambamba na kuwafuatilia kwa karibu watendaji wake ili kuimarisha kasi ya utoaji huduma.

Makamu wa Rais anaendelea na ziara yake hapo kesho Julai 9,2024 katika Manispaa ya Mji wa Kigoma kisha ataelekea wilayani Buhigwe.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa