• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

MFUMO WA M-MAMA WATAMBULISHWA KIGOMA

Posted on: April 21st, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Thobias Andengenye ameutambulisha  Mpango wa M-mama kwa Mkoa wa Kigoma wenye lengo la kupunguza vifo vya wajawazito, waliojifungua na watoto nchini  kwa kuimarisha mfumo wa rufaa na usafiri wa dharura  kwa bei nafuu kwa kutumia Teknolojia.

Utambulisho huo uliofuatiwa na kikao kazi umefanyika katika Ukumbi wa The Wallet Manispaa ya Kigoma/Ujiji na kuhudhuriwa na Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma, Wenyeviti na wakurugenzi wa Halmashauri, wawakilishi kutoka TAMISEMI, Timu ya Uendeshaji wa Huduma za Afya Mkoa, wawakilishi kutoka Vodacom Tanzania pamoja na wadau Sekta ya Afya.

Akizungumza wakati wa Kufungua kikao hicho, Mkuu wa Mkoa amewataka watendaji wote watakaohusika kusimamia utekelezaji wa wa Mpango huo kutanguliza weledi na uzalendo ili kuhakikisha malengo yaliyowekwa na Serikali yanafikiwa na kuleta matokeo chanya  katika kupunguza vikwazo wanavyopitia wanawake  kufikia huduma za uzazi stahiki.

Amesema iwapo wenye dhamana ya kusimamia na kutekeleza jukumu hilo watawajibika ipasavyo, jamii itaondokana na dhana  ya uzazi kugeuka kuwa sababu ya vifo vya mama wajawazito, wanaojifungua pamoja na watoto wachanga  kwa kuimarisha  mawasiliano na uwepo wa usafiri wa uhakika katika kata zote za mkoa wa Kigoma.

‘’Tunahitaji wataalam wajengewe uwezo na jamii ijengewe uelewa kuhusu umuhimu wa utekelezaji wa mpango huu, hali itakayosaidia kuondoa idadi ya vifo visivyo vya lazima vitokanavyo na tendo la uzazi kwa mama na watoto katika mkoa wetu’’

Aidha  Mhe. Andengenye ametoa Rai kwa Jamii mkoani hapa kutumia  fursa mbalimbali zinazotokana na utekelezwaji wa miradi mbalimbali ya huduma za Jamii kujiinua na kujiimarisha kiuchumi ili kuboresha hali zao za Maisha na Maendeleo ya Mkoa wa Kigoma kwa ujumla.

‘‘Kazi nzuri za Uboreshaji na uimarishwaji wa Miundombinu zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita tuzitendendee haki kwa kuhakikisha tunaitumia miundombinu hiyo kuimarisha mifumo yetu ya kiuchumi’’ amesema Andengenye.

Akiwasilisha Taarifa ya Hali ya viashiria vya Huduma ya Afya ya Uzazi  Mama na watoto  kwa Mkoa wa Kigoma, Mratibu wa Huduma hiyo kimkoa  Bernadetha Peter ametaja  vikwazo mbalimbali vinavyosababisha  mkwamo wa kufikia malengo ya uzazi stahiki  kwa Mkoa wa Kigoma.

Amesema kumekuwepo na hali ya ucheleweshaji wa Rufaa kutoka vituo vya ngazi ya chini vya kutolea Huduma za Afya,  ukosefu wa Elimu ya Afya na Huduma ya Uzazi miongoni mwa wanajamii pamoja na uhaba wa wataalam wenye weledi katika kutoa huduma hiyo kwa wakati.

Amezitaja sababu nyingine kuwa ni pamoja na uwepo wa tatizo la kifafa cha uzazi, kutokwa na damu nyingi wakati wa kujifungua na kuchelewa kwa  utolewaji wa Huduma za uzazi kwa wakati katika baadhi ya vituo vya kutolea huduma hiyo.

Aidha Bernadertha ametaja idadi ya vifo vitokanavyo na uzazi ambapo kwa mwaka 2018 vifo vilikuwa 78, 2029 vifo 100, 2020 vifo 119, 2021 vifo 75 na Mwaka 2022 Jumla ya vifo ilikuwa 102.

‘‘Hali ya vifo vitokanavyo na uzazi kwa mkoa wetu itapungu iwapo jamii itaupokea na kuutekeleza kwa ufanisi mfumo huu mpya wa huduma za m-mama’’ amesisitiza Bertha.

 

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa