• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

MCHENGERWA ATOA MIEZI SITA KUTOWEPO VIFO VYA MAMA WAJAWAZITO KIGOMA

Posted on: August 12th, 2024

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa (Mb) amemuagiza Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kigoma kuweka mipango madhubuti kwa kushirikiana na wataalam wa Afya ili kutokomeza vifo vya Mama wajawazito mkoani Kigoma.

Waziri Mchengerwa ametoa maelekezo hayo alipotembelea na kukagua Maendeleo ya ujenzi wa Hospitali ya Manispaa ya Kigoma Ujiji akiwa katika ziara yake ya kikazi ya Siku Tatu mkoani hapa iliyolenga kukagua utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo sambamba na kusikiliza na kutatua kero za wananchi.

‘’Nakuagiza ndani ya kipindi cha Miezi Sita kuanzia leo Agosti 12, 2024 kutoendelea kutokea kwa vifo vya wanawake wajawazito kwa sababu ambazo zinaweza kuzuilika, kwani serikali imewekeza kiasi kikubwa cha Fedha kwa ajili ya kutoa huduma bora kwa na kuzuia vifo vya mama wajawazito’’ amesema Mchengerwa.

Aidha Waziri Mchengerwa ametoa wito kwa watoa huduma za Afya nchini kuzingatia utoaji huduma bora ikiwemo kuzingatia miiko na kanuni za utumishi wao, uadilifu na kutanguliza uzalendo katika kuihudumia jamii.

‘’Sitosita kuchukua hatua za kinidhamu kwa mtumishi yeyote atakayebainika kupokea fedha kwa ajili ya kutoa huduma za Afya sambamba na kushindwa kutekeleza wajibu wake kuendana na miongozo ya utumishi wake’’ amesisitiza Waziri Mchengerwa.

Katika hatua nyingine, Mhe. Waziri amemuelekeza Mkurugenzi wa Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe OR TAMISEMI kufuatilia Fedha serikali kiasi cha Shilingi Bil.2 kwa ajili ya ukamilishaji wa majengo 16 katika Hospitali ya Manispaa ya Kigoma Ujiji.

Sambamba na agizo hilo Mchengerwa amemuelekeza Mkurugenzi huyo kufuatilia ili serikali iweze kutoa kiasi cha Shilingi Mil. 300 kwa ajili ya kukamilisha kituo cha Afya Kagunga kilichopo Halmashauri ya wilaya ya Kigoma na kukiwezesha kutoa huduma ili kuwaondolea wananchi adha ya kufuata huduma za matibabu nchi jirani ya  Burundi.

Kupitia ziara hiyo, Mhe. Mchengerwa ametoa pongezi kwa Wakala wa Barabara vijijini na Mijini (TARURA) kwa kuyaunganisha maeneo mbalimbali ya mkoa kupitia ujenzi wa madaraja ya mawe ambayo ujenzi wake hutumia gharama nafuu na kuipunguzi mzigo serikali.

Akikagua ujenzi wa barabara ya Ujiji Bangwe kwa kiwango cha Lami yenye urefu wa Km.7 inayotekelezwa chini ya mradi wa TACTICS, Mhe Mchengerwa ameonesha kutoridhishwa na mkandarasi anayetekeleza mradi huo kutokana na kuwa nyuma katika utekelezaji wa mradi tofauti kwa Asilimia 18 badala ya 60 ya mkataba wake ambapo amesisitiza kuwa serikali itafuatilia ili kuwabaini wakandarasi wote wanaochelewesha miradi ili wasipewe tena kazi za miradi kama hiyo.


Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa