• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

MASHINDANO YA UJIRANI MWEMA KUTOA FURSA KWA VIJANA KUJITANGAZA KIMICHEZO

Posted on: November 11th, 2022

Vijana mkoani Kigoma wametakiwa kujitokeza na kushiriki Mashindano ya mchezo wa soka ya Ujirani Mwema  yanayohusisha Nchi za Tanzania na Burundi ili waweze kupata fursa ya kuonyesha vipaji vyao na kufungua milango ya ajira kupitia Tasnia hiyo.

Kauli hiyo imetolewa na  Mratibu wa mashindano ya mchezo wa Soka ya Ujirani Mwema ambaye pia ni Afisa Utamaduni wa Mkoa wa Kigoma Revocatus Lutera, ikiwa ni siku chache kabla ya kuanza kwa mashindano hayo yatakayozihusisha  Timu  kutoka katika wilaya za Mkoa wa Kigoma pamoja na Mikoa ya Burundi inayopakana na Tanzania.

‘’Vijana wajitokeze wakati wa mchakato wa uundaji wa Timu hizi zinazoandaliwa kwa ajili ya kushiriki mashindano ya Ujirani mwema, hii itawapa fursa ya kutambulisha vipaji vyao na kujiweka katika Soko la mchezo huo maarufu kwa uzalishaji wa ajira ndani na nje ya nchi’’amesema.

Katika mashindano hayo, Mkoa wa Kigoma utawakilishwa na timu za Muungano kutoka Halamashauri za Kakonko na Kibondo, Kasulu na Buhigwe, Kasulu Mji na Uvinza pamoja na Halmashauri ya Mji na wilaya Kigoma.

‘‘Mashindano  yanatarajiwa kufanyika  katika Mkoa wa Makamba nchini Burundi kuanzia Novemba 14, 2022 hadi 19, 2022 yakihusisha timu nane ambapo nne ni kutoka Tanzania mkoani Kigoma na nne kutoka Burundi na mpaka sasa maandalizi yamekamilika’’ amesema Lutera.

Michezo hiyo imekuwa ni muendelezo wa utamaduni wa Ujirani mwema na kuunganisha jamii za wakazi jirani wa nchi hizi mbili kwa kuwakutanisha kila mwaka kupitia mchezo huo pendwa Duniani, ambapo zawadi za washindi hutolewa na mdhamini mkuu wa Mashindano  ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Chama Tawala nchini Burundi (CNDD-FDD) Revelian Ndikuriyo.

Aidha, mashindano hayo yaliyoanzishwa Julai 29, 2017 kupitia kikao cha Ujirani Mwema cha Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Kigoma na Mikoa ya Burundi inayopakana na Kigoma, yanalenga  kudumisha ulinzi na Usalama, kukuza urafiki, ushirikiano, upendo na undugu baina ya nchi hizi mbili.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa