• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

MAKATIBU WAKUU WA WIZARA MBALIMBALI WAKUTANA KUJADILI SUALA LA UVAMIZI WA MIFUGO HIFADHINI KIGOMA

Posted on: January 3rd, 2019

Makatibu wakuu wanne wa wizara na wataalamu mbalimbali kutoka Ofisi ya Rais Tamisemi, Wizara ya Maliasili na Utalii, Ardhi, Maendeleo ya Mifugo wamekutana mjini Kigoma kusaka suluhu ya uvamizi unaofanywa kwenye hifadhi za misitu na mapori ya akiba katika maeneo mbalimbali nchini, tatizo ambalo limekuwa likiitesa Serikali.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Prof. Adolf Mkenda ambaye ndiye Mwenyekiti wa kikao hicho, anakiri kuwapo uvamizi wa misitu wa aina tofauti unaofanywa katika namna mbalimbali, ikiwamo kuanzisha makazi na kusajili ama vijiji au vitongoji katika misitu ya hifadhi mkoani Kigoma.

Anasema, ni hali inayochangia uwepo wa uharibifu wa misitu kutoka kwa wanavijiji na wageni wanaoingia kutoka nchi jirani katika vijiji hivyo.

Profesa Mkenda anasema ufugaji holela wa mifugo ikiwamo kilimo na ufugaji holela wa kuhamahama, vijiji vingi kukosa mipango ya matumizi bora ya ardhi ni jambo jingine linalochochea uharibifu wa hifadhi za misitu.

Sababu nyingine anayotaja kuchangia uharibifu katika hifadhi za misitu nchini, ni pamoja na kuwapo mgawanyiko wa usimamizi kati ya serikali kuu na serikali za mitaa.

“Sekta ya misitu inakabiliwa na changamoto mbalimbali, ikiwamo kugawanywa kwa usimamizi wa hifadhi hizo kati ya serikali kuu na serikali za mitaa, jambo linaloleta mwingiliano wa kazi na kupishana kwa vipaumbele vya uhifadhi. Hata suala la ufugaji Mkoa wa Kigoma ni tishio Zaidi kwa ustawi wa misitu,” anasema Profesa Mkenda.

Anafafanua kwa kusema ufugaji ndani ya misitu mkoani Kigoma unafanywa na wenyeji na watu kutoka nchi jirani wakifanya kazi hiyo kwa kushirikiana.

Profesa Mkenda anasema kutokana na chanagmoto hizo Serikali imeamua kuchukua hatua za kuhakikisha wanakomesha vitendo hivyo kwa nguvu zote kwa kukutanisha makatibu wakuu wa Wizara zote zinazohusika.

Anasema kazi yao nikutoa mapendekezo kwa mawaziri wa wizara husika juu ya namna bora ya kumaliza tatizo la wafugaji kuvamia misitu kwa kuzingatia masilahi mapana ya taifa. Ripoti ambayo wataikabidhi Januari 04, 2018.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Elisante Ole Gabriel, amekiri kutambua tatizo la wafugaji kuvamia hifadhi za misitu na kuwataka wafugaji hao kujiandaa na kutii maamuzi yatakayotolewa na Serikali.

Mtendaji Mkuu wa TFS, Profesa Dos Santos Silayo anataja mbinu zinazotumika kudhibiti uhariubifu wa misitu kuwa ni ulinmzi shirikishi ambapo TFS hushirikiana na wanachi kupambana na hali hiyo, matumizi ya intelijensia kuzuia uhalifu, pamoja kuimarisha ushirikiano wa kikanda na nchi jirani.


Makatibu Wakuu wengine waliohudhuria kikao hicho ni Naibu Katibu Mkuu kutoka Ofisi ya Rais Tamisemi, Tixon Nzunda na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mathias Kabunduguru.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa