• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

MAJALIWA AHIMIZA KILIMO CHA MAZAO YA KIMKAKATI

Posted on: February 26th, 2023


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa (Mb) amesema Serikali itanedelea kuhamasisha na kusimamia kilimo cha mazao ya kimkakati nchini ikiwemo zao la chikichi ili kuboresha maisha ya wananchi na kuimarisha uchumi wa Taifa.

Waziri Majaliwa ametoa kauli hiyo alipoongoza kikao kazi kilichowawakutanisha wadau wa zao la Chikichi Mkoani Kigoma, kilicholenga kufanya Tathimini ya mafanikio pamoja na kuweka mikakati ya kuboresha kilimo cha zao hilo.

Amesema Serikali imeamua kuongeza nguvu katika uwekezaji wa Kilimo cha chikichi kwa lengo la kuhakikisha kunakuwepo na utoshelevu katika upatikanaji wa mafuta ya kula nchini ili kuipunguzia  Serikali mzigo wa kuagiza huduma hiyo muhimu nje ya nchi.

‘‘Viongozi wa Serikali hakikisheni mnawaelimisha wananchi, kuwasaidia kupata miche na kuwajengea uelewa kuhusu umuhimu wa kilimo cha zao la chikichi katika maeneo yenu ili waweze waweze kujiinua kiuchumi na kuongeza upatikanaji wa huduma ya mafuta ya kula yanayotengenezwa ndani ya nchi’’ Amesema Majaliwa.

Ameongeza kuwa, Serikali itaendelea kuimarisha vituo vya utafiti wa mbegu bora za Chikichi ndani na nje ya Mkoa wa Kigoma, kwa lengo la kuongeza uzalishaji utakaowaletea tija wananchi.

Aidha Majaliwa amesisitiza taasisi za kifedha kuendelea kutoa mikopo kwa Wananchi wanaojishughulisha na kilimo cha zao hilo pale watakapothibitika kukizi vigezo vya kupata mikopo hiyo.

Akiwasilisha Taarifa ya hali ya uzalishaji na usambazaji wa chikichi aina ya TENERA nchini, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo nchini (TARI) Mhandisi Geofrey Mkamilo amesema hadi kufikia Februari 2023, miche 621,213 yenye Thamani ya Shilingi Bil 1.7 imegawiwa bure ndani na nje ya Mkoa wa Kigoma kwa lengo la kuimarisha kilimo cha zao hilo la kimkakati.

Amefafanua kuwa, katika upandaji wa zao la chikichi, Mkoa wa Kigoma ni wapili kitaifa  ambapo wakazi wamefanikiwa kupanda miche 58,445 ambayo imepandwa katika Ekari 1,124 huku Halmashauri ya wilaya na Mji Kasulu ikiongoza kwa wananchi kupanda miche bora 42,582 katika eneo lenye ukubwa wa Jumla ya Ekari 819.

Upande wao wadau kutoka Taasisi za kifedha mkoani Kigoma waliopata fursa ya kushiriki kikao hicho, wamesema wanaendelea kutoa mikopo kwa wakulima wa zao la chikichi ili kuhakikisha wanafikia malengo waliyojiwekea kupitia kilimo na uchakataji wa zao la chikichi.

Aidha wameiomba Serikali kuweka utaratibu mzuri kwa ajili ya kutatua changamoto mchakato wa masherti na vigezo vya Dhamana baina ya wakulima na Taasisi hizo ili kurahisisha zoezi la utoaji wa Mikopo kwa wakulima.

Baadhi ya wadau wa Kilimo cha zao la chikichi waliojitokeza na kushiriki kikao kazi hicho wamemshukuru Waziri Mkuu kwa kujikita katika kuhamasisha na kusimamia kilimo cha zao  hilo mkoani Kigoma na kusisitiza kuwa, wameanza kuona faida zake kiuchumi na ushirikiano mkubwa kutoka Serikalini.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa