• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA WAANZA KAMBI YA SIKU SITA MKOANI KIGOMA

Posted on: October 7th, 2024

 

Madaktari bingwa wa Dkt. Samia wameanza Kambi maalum ya Matibabu ya Kibingwa mkoani Kigoma ambapo wataanza kutoa Huduma za kiafya kwa Siku Sita kuanzia leo Oktoba 7, 2024 katika Hospitali Nane (8) za Halmashauri za Mkoa wa Kigoma.

Akizungumza mara baada ya kuwapokea madaktari hao, Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma Hassan Rugwa amesema wananchi wanapaswa kutumia fursa ya uwepo wa madaktari hao kwa lengo la kupata matibabu ya kibingwa jirani na maeneo yao badala ya kuyafuata katika Hospitali za mbali hivyo kuokoa muda na gharama kubwa pamoja na usumbufu wa kusafirisha wagonjwa wao.

Mhe. Rugwa amewataka madaktari hao kubaini changamoto za kimatibabu zilizopo mkoani Kigoma na kutoa ushauri namna bora ya kuzikabili ili kuimarisha utoaji wa huduma mkoani Kigoma kupitia maboresho ya sera za huduma za Afya.

‘’Mkoa wa Kigoma ni miongoni mwa mikoa inayopakana nan chi jirani hivyo mnapoenda kutoa huduma muutumie muda huo kubaini maradhi ambayo hayapo maeneo mengine ya nchi ili kwa pamoja tuweze kuyadhibiti yasiweze kusambaa katika mikoa mingine’’amesema Rugwa.

Aidha Katibu Tawala ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuendelea kusogeza huduma mbalimbali ikiwemo huduma za Afya kwa wakazi mkoani Kigoma na Tanzania kwa ujumla na kuwarahisishia wananchi utatuzi wa changamoto mbalimbali zinazohusu afya zao.

Jackline Ndanshau Mwakilishi kutoka Wizara ya Afya amesema kambi hiyo ya Madaktari wa Samia itafanyika kwa muda wa siku sita kuanzia Oktoba 7 hadi 12,2024 na itahusisha Hospitali zote za Halmashauri  ambapo kila kituo kitapokea madaktari saba (7) ikiwa ni Daktari Bingwa wa magonjwa ya wanawake na uzazi, watoto na watoto wachanga, usingizi na ganzi, magonjwa ya ndani, upasuaji na mfumo wa mkojo pamoja na muuguzi bingwa.

Amefafanua kuwa upande wa Hospitali za Halmashauri za Mjini(karibu na Hospitali za Rufaa na za Mkoa) watapokea pia daktari bingwa wa mifupa hivyo maeneo hayo timu itakuwa na jumla ya wataalam nane(8).

Ndanshau ameeleza kuwa lengo la serikali ni kusogeza huduma bobezi na zile za kibingwa katika Halmashauri zote 184 nchini, kuimarisha ujuzi wa wataalam wa Afya waliopo kazini sambamba na kuimarisha na kuanzisha wodi maalum za watoto wachanga wagonjwa na waliozaliwa na uzito pungufu.

PICHA ZA PAMOJA.


Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa