• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

MABARAZA YA KATA YAASWA KUTOJIHUSISHA NA UTOAJI HUKUMU

Posted on: December 6th, 2022

Wajumbe wa Mabaraza ya Kata Mkoani Kigoma wametakiwa kutekeleza majukumu yao ya kisheria kwa kujikita katika kusuluhisha mashauri  mbalimbali yanayojitokeza katika Jamii zao huku wakijiepusha na jukumu la kutoa hukumu juu ya mashauri hayo kwani kufanya hivyo ni kuingilia majukumu ya kimahakama.

Kauli hiyo imetolewa na Kaimu Katibu Tawala Msaidizi Mipango na Uratibu Mkoa wa Kigoma, Msafiri Nzunuri alipokuwa akizungumzia kuhusu Maadhimisho ya Wiki ya Msaada wa Kisheria yanayotarajiwa kufanyika kimkoa wilayani Kibondo.

Amesema baadhi ya wajumbe kwa kushirikiana na watendaji hujikuta wakikiuka sheria na mipaka ya utendaji kazi wao kwa kutoa hukumu za mashauri wanayopelekewa na wananchi katika maeneo yao, huku wakijua wazi kuwa jukumu hilo kisheria linatekelezwa na ngazi mbalimbali za kimahakama.

‘‘Hukumu yoyote inapotolewa kisheria huzingatia vifungu vya Sheria, utoshelevu wa ushahidi kutoka pande zote mbili pamoja na kusimamiwa na watu wenye weledi kwa kuwa na Taaluma ya Sheria’’ amesema.

Amesisitiza kuwa, jukumu la msingi la mabaraza ya kata kiusuluhishi kwa kushirikiana na watendaji wa kata ni kulinda amani na utulivu  kwa kuwasaidia  wahusika wa migogoro  kufikia muafaka katika ngazi ya kata husika. Aidha migogoro hiyoisuluhishwe kwa njia za kirafiki pande zote zote mbili za mgogoro.

Kuhusu Maadhimisho ya wiki ya msaada wa kisheria, Msafiri amesema utungaji wa Sheria Namba 1 ya Mwaka 2017 unalenga kuongeza upatikanaji wa Haki kwa wote huku ukiwajumuisha watu wenye uwezo duni wa kupata huduma za kisheria kwa mawakili kutokana na kushindwa kumudu gharama.

Amefafanua kuwa, Maadhimisho hayo yamelenga kuongeza uelewa wa kisheria  kwa jamii juu ya haki za watoto, wanawake na makundi mengine yanayolengwa kwa  lengo la kukomesha unyanyasaji wa kijinsia na ukatili nchini kote kwa kuongeza upatikanaji wa huduma za msaada wa kisheria.

Maadhimisho ya wiki ya msaada kisheria yanafanyika kwa wiki moja kuanzia tarehe 5 hadi 10 Desemba 2022 nchini kote yakilenga kutoa elimu ya kisheria, kupokea na kutatua malalamiko ya kisheria, kubainisha maeneo ya huduma za kisheria, kuendesha kampeni za hamasa kwa Umma kuhusu umuhimu wa kutumia msaada wakisheria pamoja na kutoa huduma ya msaada wa kisheria kwa watu walioko maeneo ya vizuizi.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AZINDUA RASMI ZOEZI LA UGAWAJI VYANDARUA KIMKOA

    May 27, 2025
  • JAMII INAPASWA KUZINGATIA CHANJO KUJILINDA NA MARADHI

    May 20, 2025
  • MRADI WA UHIFADHI MAZINGIRA WAZINDULIWA KIGOMA

    May 15, 2025
  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa