• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

MABARAZA YA BIASHARA YATUMIKE KUPANGA MIKAKATI YA KIBIASHARA BADALA YA KUTATUA MIGOGORO PEKEE- RC ANDENGENYE

Posted on: July 31st, 2024

Wafanyabiashara mkoani Kigoma wametakiwa kutumia fursa ya uwepo wa mabaraza ya Biashara kwa ajili ya kuweka mikakati ya kuibua fursa mpya za kiabiashara badala ya kutumika kwa ajili ya kutatua migogoro ya wafanyabiashara pekee.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Thobias Andengenye alipozungumza wakati akifungua Mkutano wa Baraza la Biashara Mkoa wa Kigoma uliofanyika katika Hoteli ya Lake Tanganyika iliyopo Manispaa ya Kigoma Ujiji na kusisitiza kuwa  serikali itaendelea kuimarisha Mazingira ya uwekezaji mkoani Kigoma ili kutimiza dhamira ya Mhe. Rais ya Dkt. Samia Suluhu ya kuufanya mkoa kuwa kitovu cha Biashara kwa ukanda wa Magharibi.

Amesema ili kuleta tija kibiashara mikutano ya mabaraza ya biashara isitumike kutatua changamoto za wafanyabiashara pekee bali iweke mikakati ya pamoja katika kuibua fursa za kibiashara na uwekezaji ili kuinua uchumi wa mkoa na Taifa kwa ujumla.

‘’Iwapo mikutano hii itafanyika mara kwa mara, itaondoa migogoro isiyo ya lazima na kutuepusha migomo ya wafanyabiashara inayoweza kujitokeza  kutokana na changamoto zilizopo kupata utatuzi kwa wakati  hii’’ amesema Andengenye.

Amesema Serikali imeelekeza zaidi ya Shilingi Tri. 8 kwa ajili ya kuimarisha miundombinu ya uchukuzi na usafirishaji mkoani Kigoma sambamba na kufanya ukarabati wa meli za Mt. Sangara, MV Liemba pmaoja na Mwongozo kwa ajili ya kujenga mazingira rafiki kwa wafanyabiashara na wawekezaji wa ndani na nje ya mkoa wa Kigoma kusafiri wao wenyewe na kusafirisha bidhaa zao.

‘‘Serikali ya awamu ya Sita inaendelea kuimarisha upatikanaji wa huduma ya umeme wa uhakika wa Gridi ya Taifa , kuboresha uwanja wa ndege pamoja na ujenzi wa barabara zinazouunganisha mkoa na mikoa ya jirani kwa kiwango cha Lami’’ amesema Mkuu wa Mkoa.

Aidha Mwenyekiti wa kikao hicho ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Kigoma amesema Serikali itaendelea kupokea na kufanyia kazi maoni ya wafanyabiashara  pamoja na kutatua changamoto zao kwa haraka ili kuwawekea mazingira rafiki  wafanyabashara  na kuwawezesha kufikia malengo waliyojiwekea.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa