• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

MAAFISA UTUMISHI WATAKIWA KUTOKUWA KIKWAZO KWA WATUMISHI WA UMMA

Posted on: December 16th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye amewataka Maafisa Utumishi katika Halmashauri mkoani humo kushughulikia changamoto za kiutumishi zinazowakabili watumishi wa Umma ili kuondoa manung’uniko yanayochangia kushusha ari ya kiutendaji kwa wafanayakazi.

Ujio wa kauli hiyo umefuatia Mkuu huyo wa Mkoa kukutana na watumishi wa Umma katika  Halmashauri ya wilaya ya Kakonko akiwa kwenye ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua miradi ya Maendeleo, kusikiliza na kutatua kero za wananchi.

‘’ Msiruhusu watumishi wa Umma wakaacha majukumu yao kwa lengo la kuwafuata kwenye ofisi zenu, hali hii inasababisha kupoteza muda mrefu wanaopaswa kuutumia kutekeleza majukumu yao’’alisema.

‘’Mnafahamu dhamana yenu katika utumishi wa Umma hivyo wapunguzieni kazi ya kuhangaika kutafuta viongozi au watu wa kuwasaidia kutatua matatizo ambayo yapo chini ya uwezo wenu’’ alisistiza Andengenye.

Katika kuhakikisha agizo hilo linafanikiwa kiutekelezaji Mkuu huyo wa Mkoa amewaelekeza wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha wanawawezesha maafisa utumishi  kuwafikia watumishi wa Umma katika maeneo ya kazi ili kuwasikiliza na kutatua changamoto zinazohitaji miongozo ya kiutumishi.

Akizungumzia utendaji kazi wenye tija, kiongozi huyo amewataka watumishi wa Umma mkoani hapa kudumisha uadilifu, nidhamu na kujituma ili waweze kupata matokeo makubwa katika utendaji kazi wao.

‘’Niwasihi tuendelee kuiunga mkono serikali ya awamu ya sita kwa kutangaza kazi nzuri zinazofanywa na Mhe. Rais Samia Suluhu huku tukikumbuka sisi sote ni wasaidizi wake katika kuwatumikia wananchi na kuliletea Maendeleo Taifa letu’’ ameongeza.

‘’Mkitumia vibaya nafasi zenu mtaleta matokeo hasi kwa Taifa letu hivyo shirikianeni, pokeeni ushauri na maelekezo kutoka kwa viongozi wenu pamoja na kutanguliza uzalendo katika utendaji kazi wetu’’ametahadharisha Mkuu huyo wa Mkoa.

Kupitia ziara hiyo, Mkuu huyo wa Mkoa amekagua ujenzi wa Shule ya Sekondari Rutenga inayojengwa kwa fedha kiasi cha Shilingi 603,890,562 kutoka Serikali Kuu pamoja  ujenzi wa miundombinu katika shule ya msingi Nyamwilonge chini ya Mradi wa BOOST kwa Thamani ya shilingi 110,600,000 pamoja na Shule ya Kumkobe Shilingi 361,500,000.

Upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Ndaki Mhuli amesema kukamilika kwa shule hizo kutapunguza Adha ya wanafunzi kutembea umbali mrefu kufuata huduma za kielimu.

Pia Ndaki amewataka wazazi katika kata ya Nyamtukuza kutumia miundombinu hiyo kuendana na malengo ya serikali ili kuhakikisha watoto wote katika maeneo hayo wanapata elimu bora.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa