• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

MAADHIMISHO YA NANENANE YAENDELEE KUTUMIKA KAMA SOKO NA DARASA HURIA KWA WAZALISHAJI

Posted on: August 11th, 2025



Na. Clinton Justine-Kigoma.

Maonesho ya Nanenane Kanda ya Magharibi yaliyohusisha Mikoa ya Tabora na Kigoma yamehitimishwa Tarehe 8, Agosti, 2025 ambapo kutokana na umuhimu wake, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma  Mhe. Balozi Simon Sirro aliongeza Siku mbili ili wadau wa maonesho hayo kupata fursa Zaidi ya kunufaika na tukio hilo.

Kupitia maonesho hayo imeshuhudiwa wafugaji, wakulima, wadau wa uvuvi, mashirika, Kampuni na Taasisi mbalimbali za kibiashara na kifedha pamoja na wajasiriamali  wakijumuika kuonesha, kutangaza na kuuza  bidhaa zao sambamba na kutoa maelekezo ya namna huduma wanazotoa zinavyoweza kuleta mapinduzi katika maisha ya kila siku ya binadamu.

Pamoja na yote hayo, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma akiwa mgeni rasmi katika kufunga maonesho hayo amesisitiza mambo kadhaa ikiwemo suala la kuanzishwa kwa madarasa maalum yatakayohusisha wataaalam kutoka Idara, vitengo au ndani ya Sekta mbalimbali kwa lengo la kuwakutanisha pamoja wananchi na kuwafundisha namna bora ya kutekeleza majukumu  yao kuendana na Sekta waliyojikita kiuzalishaji.

Anasema mfano; kukiwa na eneo maalum la darasa, wahitaji wataenda hapo na kupatiwa mafunzo bobezi ndani ya siku husika za maonesho. Mfano Idara ya Uvuvi itaandaa mtaalam bobezi kutoka katika Wizara hiyo naye atatengewa eneo maalum kwa ajili ya kuwafundisha wadau wa uvuvi hatua kwa hatua na kwa kina kuhusu shughuli za uvuvi wanazozifanya ili nao wakitoka hapo waweze kwenda kuwa walimu wazuri kwa jamii katika maeneo yao ya uzalishaji.

Anasema sambamba na hayo, Halmashauri zinapaswa kuandaa utaratibu wa kuchukua sampuli za wadau wa nanenane kama wafugaji, wafanyabiashara wadogowadogo, wazalishaji wadogo au wale wa kati na hata wakulima kisha kuwaweka kwenye madarasa hayo ili kuwajengea uwezo kwa makubaliano ya kwenda kutoa elimu hiyo katika maeneo yao.

Pamoja na hayo, Mkuu wa Mkoa ameenda mbali Zaidi kwa kuzitaka halmashauri na taasisi zinazohusika katika shughuli za maonesho katika maeneo yao kuhakikisha zinajenga miundombinu ya kudumu na yenye mifumo rafiki kwa ajili ya kazi wanazozifanya.

Aidha kupitia hotuba aliyoitoa kwenye kilele cha maadhimisho hayo, Mhe. Balozi Sirro ametoa wito kwa wakulima wafugaji na wavuvi  kuongeza kasi ya matumizi ya teknolojia, zana bora na za kisasa pamoja na kujifunza na kwenda sambamba mnbcxvz na mifumo ya kisasa ya ufugaji ili kuongeza tija katika uzalishaji.

Aidha Balozi Sirro amezungumzia umuhimu wa kuboresha kwa kiasi kikubwa mifumo ya uandaaji wa vifungashio ili kuziweka bidhaa katika hali ya kuhimili ushindani wa kimasoko. Anasema iwapo bidhaa zinazozalishwa na kuingizwa katika soko la dunia hazitokuwa na vifungashio vyenye kuzitambulisha bidhaa hizo zitakosa soko la uhakika na zitaishia kuuzwa katika soko la ndani.

‘’Nitumie nafasi hii kutoa wito kwa wenzetu wa Shirika la Viwango Tanzania(TBS) kuona namna bora ya kushiriki maadhimisho haya kwa mwaka ujao ili watupe mkakati na kutoa Elimu ya namna bora ya kupata huduma ya wataalam wa vifungashi na kuziwezesha bidhaa zetu kuingia katika masoko makubwa ya ndani sambamba na kuleta ushindani katika Soko la Dunia’’ ameshauri Sirro.

Kwa kuongezea amezitaka Halmashauri kwa kushirikiana na wataalam wa Sekta ya Biashara, Viwanda na Uwekezaji kuanza mchakato wa kuwajengea uwezo wananchi wazalishaji kuhusu umuhimu wa kutumia vifungashio vinavyokidhi viwango vya kimataifa sambamba na kuwakutanisha na wataalam watakaowasaidia namna bora ya kufanikisha upatikanaji wa wataalam wanaohusika na zoezi hilo.

Awali Hassan Rugwa ambaye ni Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma alitembelea mabanda hayo na kuzungumza na wadau wa nanenane ambapo aliwasisitiza kuhakikisha wanatumia fursa ya maonesho hayo sio tu kwa kutangaza bidhaa zao bali kuziuza.

‘’Kiuhalisia ili tufikie malengo yetu ni lazima bidhaa tunazoleta kuzitangaza ziwe na ubira na zenye utofauti ili ziweze kumudu ushindani wa kimasoko sambamba na kuuzika kwa wingi. Mtakapokuja tena kwenye maonesho haya mwaka ujao hakikisheni mnasafirisha bidhaa zenu kwa ajili ya kuziuza pia badala ya kuishia kuzitangaza’’ ameshauri Rugwa.

Kuhusu ushindani wa kimasoko, Katibu Tawala huyo amewataka wataalam wa Halmashauri katika Sekta ya Biashara kuzidi kutumia teknolojia ya kisasa kutafuta masoko ya ndani na nje ya nchi ili kuwapunguzia adha wananchi wazalishaji mali ambao wanauhitaji mkubwa wa amsoko hayo kutokana na kufanikia katika uzalishaji  wa bidhaa.

Mkoa wa Kigoma na Tabora kwa ujumla ni mikoa yenye kiwango kikubwa cha uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara kwa wingi sambamba na uwepo wa mazao ya uvuvi pamoja nay ale yatokanayo na Nyuki. Mazao haya yameendelea kuwa na soko kubwa ndani nan je ya nchi, hivyo Rai ya Mkuu wa Mkoa kuhusu matumizi ya vifungashio sahihi na vyenye kukidhi viwango vya kimataifa ni jambo lisilokwepeka ili kuinua pato na kuleta matokeo chanya kwa mkulima.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • UJENZI KITUO CHA AFYA MAKERE WAFIKIA ASILIMIA 70

    August 27, 2025
  • UJENZI KITUO CHA AFYA RUKOMA KUWAONDOLEA ADHA WAKAZI KUFUATA HUDUMA ZA AFYA ZAIDI YA KM 10

    August 25, 2025
  • MRADI WA AFYA HATUA KUONGEZA KASI MAPAMBANO DHIDI YA UKIMWI MANISPAA YA KIGOMA UJIJI

    August 18, 2025
  • MRADI WA AFYA HATUA KUONGEZA KASI MAPAMBANO DHIDI YA UKIMWI MANISPAA YA KIGOMA UJIJI

    August 18, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa