• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

WIZARA YA FEDHA KUTOA ELIMU YA FEDHA KIGOMA

Posted on: June 3rd, 2024

Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma Hassan Rugwa ameitaka Jamii mkoani hapa kuchangamkia fursa ya Elimu ya Fedha inayotolewa na Serikali kupitia Wizara ya Fedha ili kuwajengea wananchi uelewa na kudhibiti athari za kiuchumi zitokanazo na ukosefu wa Elimu ya uwekezaji, utunzaji wa akiba na mikopo isiyo na tija.

Rugwa ametoa wito huo alipokutana na kufanya mazungumzo na wataalam kutoka Wizara ya Fedha kwa kushirikiana na OR-TAMISEMI waliopo mkoani hapa kwa lengo la kutoa mafunzo ya Elimu ya Fedha kwa makundi mbalimbali ikiwemo wafanyabiashara, watumishi wa Umma na Sekta Binafsi, wajasiriamali, watoa huduma za kifedha, wawekezaji,  SACCOS, vikundi vya kifedha vya kijamii pamoja na wanufaika mbalimbali wa huduma za kifedha mkoani hapa.

Amesema Elimu ya Fedha ni suala muhimu kwa kila mnufaika wa fedha ili kupata ujuzi wa kuhifadhi, kuziendeleza, kufahamu Sheria za biashara, ulipaji kodi, taratibu za uwekezaji na upatikanaji wa hisa sambamba na kufanya matumizi binafsi yatakayolenga kuheshimu matumizi bora ya fedha.

Ameeleza kuwa, kuna umuhimu mkubwa kwa wananchi kupata ujuzi wa Elimu ya Fedha na Biashara, ili kuwajengea uwezo na kuwaongezea ubunifu wananchi katika kufanya biashara pamoja na uwekezaji na kujiongezea kipato hali itakayosaidia kuepuka hasara zisizo za lazima.

‘’Kigoma ni miongoni mwa mikoa inayotoa idadi kubwa ya wajasiriamali ndani na nje ya mkoa hivyo suala hili limekuja katika muda sahihi kwani itasaidia kuwajengea uelewa wale walipo kwenye biashara katika ngazi mbalimbali pamoja na wanaofikiria kuanzisha biashara’’ alisema Rugwa.

Upande wake Afisa Usimamizi wa Fedha kutoka Wizara ya Fedha Stanley Kibakae amesema lengo ni kutembelea na kukutana na wanufaika wa fedha katika Halmashauri zote za Mkoa wa Kigoma  ili kuwajengea uwezo watoaji na wapokeaji wa huduma za kifedha.

Amefafanua kuwa mkoa wa Kigoma hali ya uelewa wa masuala haya ya kifedha ipo chini ndio maana Wizara imechukua hatua ya kutuma wataalam watakaokutana na  wadau wa fedha na kuhakikisha Elimu inayotolewa inabadilisha mitazamo na uelewa wa kifedha kwa makundi mbalimbali.

Amesema Elimu ya fedha ni Taaluma ya kielimu kama zilivyo elimu nyingine hivyo lengo ni kuleta mabadiliko, aidha amesisitiza kuwa, utoaji wa elimu umerahisishwa ili kila atakayefikiwa aweze kuwa na uelewa na kumudu kuendana na Sheria ya huduma ndogo za kifedha ya Mwaka 2018 na kanuni yake ya Mwaka 2019.

‘’Kuna baadhi ya watoa huduma za kifedha wanakumbwa na changamoto za kukosa uelewa wa masuala yakifedha au kukosa uaminifu jambo linalosababisha kutoza riba kuwa na kuweka masharti yasiyo rafiki na kandamizi dhidi ya wapokea huduma za kifedha’’ alisema Kibakae.

Ameongeza kuwa elimu hiyo ni muhimu ili kuhakikisha wanufaika wa kifedha wanafanikiwa kuweka akiba, kufanya uwekezaji, kufahamu taratibu za kulipa kodi sambamba na kutoa fursa kwa wafanya kazi kujiandaa na maisha baada ya kutamatika kwa muda wao wa kiutumishi.

Kadhalika kupitia maarifa hayo ya kifedha, watoa huduma za kifedha watasajiliwa na kutambuliwa rasmi,watendana na sharia za nchi zinazoongoza taratibu za kifedha, ‘’nitoe wito kwa wajasiriamali na wafanyabiashara mkoani Kigoma kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa kuendana na sheria ndogo za fedha’’ alisisitiza Kibakae.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AZINDUA RASMI ZOEZI LA UGAWAJI VYANDARUA KIMKOA

    May 27, 2025
  • JAMII INAPASWA KUZINGATIA CHANJO KUJILINDA NA MARADHI

    May 20, 2025
  • MRADI WA UHIFADHI MAZINGIRA WAZINDULIWA KIGOMA

    May 15, 2025
  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa