• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

LINDENI MIUNDOMBINU YA MAJI ILI TUWE NA MIRADI ENDELEVU-RC ANDENGENYE

Posted on: March 6th, 2023

Wakazi katika Manispaa ya Kigoma/Ujiji wametakiwa kutunza na kuilinda Miundombinu ya Maji iweze kudumu na kuinufaisha Jamii kwa Muda mrefu ili Fedha zinazotengwa kwa ajili ya ukarabati zikatumike kuendelezana kuibua  miradi mingine.

Miundombinu ya Maji iliyopo ikitumiwa kwa usahihi na kuiepusha na uharibufu, itaruhusu pesa zilizotengwa kwa ajili ya ukarabati kutumika katika kuendelea kuisogeza huduma hiyo muhimu katika maeneo ambayo hayajafikiwa na kuzidi kuigusa idadi kubwa ya wananchi.

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Thobias Andengenye amesema hayo alipotembelea Mradi wa Ujenzi wa chanzo cha Maji cha Amani Beach akiambatana na Katibu Tawala pamoja na Kamati ya Ulinzi Mkoa, kwa lengo la kujionea maendeleo ya ujenzi wa Chanzo hicho kipya cha Maji katika Manispaa ya Kigoma/Ujiji.

Amesisitiza kuwa iwapo miundombinu hiyo itatunzwa, Marekebisho yatafanyika katika maeneo yenye uchakavu na ubovu na sio kwa sababu ya uharibifu wa makusudi unaofanywa na watu wachache wenye nia ovu dhidi ya mipango ya Maendeleo ya Serikali.

‘Tukiilinda na kuitunza miundombinu tuliyonayo, tutapunguza gharama za kuendesha mradi na kupanua wigo wa utoaji wa huduma, hivyo yeyote atakayebainika kufanya uharibifu hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yake ili iwe fundisho kwa wengine wenye tabia kama hizo’’ amesisitiza Andengenye.

Aidha Mkuu wa Mkoa amesisitiza kuwa, kukamilika kwa mradi huo kutaongeza fursa ya wananchi kuunganishwa katika mfumo wa Huduma ya Maji na kutimizwa kwa azma ya Mhe. Rais Dkt. Samia ya kumtua mama ndoo kichwani.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Manispaa ya Kigoma/Ujiji Mha. Mbike Jones amesema mradi huo umekamilika na tayari unazalisha lita Mil. 23 kwa siku huku mahitaji halisi ikiwa ni Lita Mil. 23 hivyo kufanya uzalishaji kufikia Asilimia mia moja.

Amefafanua kuwa Mradi huo ulianza kutekelezwa Julai 2021 na na kukamilika Januari 2023 chini ya Mkandarasi Sinohydro Corporation Ltd, unauwezo wa kuzalisha Mita za ujazo 42,000 kwa siku na unanufaisha takribani watu 384,000 wakazi wa Manipsa ya Kigoma/Ujiji na maeneo ya Jirani.

Aidha amewasisitiza wateja wa Huduma hiyo  kulipa madeni ya Huduma ya Maji wanayodaiwa kwa wakati ili kuruhusu uendeshaji  wa uhakika wa Mradi huo.

‘‘wateja wetu wanapolipa madeni yao Fedha tunayoipata inatuwezesha kununua vipuri, kukarabati mitambo pamoja na miundombinu ili kuifanya huduma ya Maji kuwa ya uhakika’’ amesisitiza Mha. Mbike.

Pia Mha. Mbike amefafanua kuwa hali ya kuwepo kwa mgao wa Maji kwa Baadhi ya maeneo inatokana na mabomba kutokuwa na uwezo mkubwa wa kupitisha maji hivyo katika kutatua changamoto hiyo, mamlaka inampango wa kuyafikia kisha kuyatambua maeneo hayo kwa lengo la kubadilisha aina ya mabomba yanayotumika.

‘‘Nitoe Rai kwa wananchi wote wenye uhitaji wa huduma ya Maji watume maombi katika sehemu husika ili waweze kupatiwa huduma hiyo kwani uzalishaji ni toshelevu na unaendana na idadi halisi ya mahitaji katika manispaa ya Kigoma/Ujiji na maeneo jirani’’ amesema Mhandisi Mbike.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa