• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

MKUU WA MKOA AAGIZA WALIOISABABISHIA HATI CHAFU MANISPAA YA KIGOMA UJIJI WACHUKULIWE HATUA

Posted on: August 3rd, 2017

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Brigedia Jenerali (Mst.) Emmanuel Maganga ameuagiza uongozi wa Manispaa ya kigoma/ ujiji kuwachukulia hatua za kisheria watumishi waliohusika katika ubadhirifu na wizi wa fedha na kupelekea Manispaa hiyo kuwa na hati chafu kwa mfululizo wa miaka miwili 2014/2015 na 2015/2016.

Mhe. Maganga ameagiza kuwu tarifa ya hatua za kinidhamu na kiutawala iwasilishwe katika ofisi ya Katibu Tawala wa Mkoa ndani ya Miezi Miwili kuanzia leo yaani siku 60.

Akizungumza katika Kikao cha Baraza la Madiwani katika Manispaa ya Kigoma Ujiji Mkuu wa Mkoa Maganga amesema malalamiko na migogoro mingi inasababishwa na utendaji mbovu wa baadhi ya watendaji na watumishi na wengine wakijificha katika mgongo wa madiwani katika kutenda kinyume na taratibu za kiutumishi.

Mwenendo wetu kiutendaji haubadiliki tunapaswa kubadilika ili kuleta matokeo chanya kwa wananchi. Waheshimiwa madiwani na watendaji tufanye kazi kwa malengo na zejye kupimika. Aliongeza Maganga.

Aidha Maganga ametoa maelekezo mbalimbali ikiwemo kuacha kutengeneza shughuli nje ya bajeti iliyoidhinish, madiwani kuacha kujihusisha na masuaa ya utendajimathalani zabuni na biashara na Halmashauri pamoja na kujiepusha kuingila michakato ya zabuni inayoendeshwa na Bodi ya Zabuni ya Manispaa ya Kigoma Ujiji.

Zipo taarifa kuwa baadhi ya madiwani wanalinda watumishi wasio waadilifu ili wasichukuliwe hatua za kisheria na kinidhamu pindi wanapogundulika na makosa hili haikubaliki kabisa alisisitiza Brigedia Jenerali Maganga.

Amekemea vikali suala la watendaji na watumishi kujihusisha na malipo yasiyofuata taratibu za sheria ya fedha.Aidha amewataka kusingatia hoja na maelekezo ya Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ili kuondokana na kupata hati chafu. Amesema haiwezekani hoja zote saba zikepelekea kupata hati chafu kwa miaka miwili mfululizo hali hii haivumiliki, wote waliohisika wawe wamehama katika Manispaa hii au wamestaafu watafutwe na waletwe kujibu hoja hizi.

Mhe. Mkuu wa Mkoa amevielekeza vyombo husika kuharakisha upelelezi ili hatua stahiki zichukuliwe kwa watakaobainika kutenda makosa hayo.

Kikao cha Baraza la Madiwani wa Manispaa ya Kigoma Ujiji ambacho kilikuwa na agenda mojo tu ya Hoja za  Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikalikilihudhuriwa pia naZito Zuberi Kabwe ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Kigoma mjini amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Kigoma kwa kutoa maagizo na maelekezo mbalimbali na kuomba yasimamiwe na yatekelezwe ili kuondoa aibu ya Manispaa ya kupata hati chafu.

Mhe. Zitto amesema yeye hatamwonea aibu Mtumishi au diwani yeyote anayekwamisha maendelo ya Manispaa. Amewataka madiwani bila kujali itikadi ya vyama kuunga mkono jitihada za serika za maendeleo kwa wananchi, pia kutooneana aibu kwa wanaokwenda kinyume na taratibu ikiwemo wizi na ubadhirifu wa fedha za umma.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa