• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

KUKAMILIKA MIRADI YA UMEME KUTAONGEZA FURSA ZA UWEKEZAJI KIGOMA

Posted on: August 16th, 2022


Dkt. Suleiman Daud akitoa neno la shukurani kwa Mkuu wa Mkoa wa Kigoma( hayupo pichani) Mara baada ya kumaliza mazungumzo mafupi yaliyofanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kigoma. Dkt Daudi akiambatana na wataalam kutoka  katika Taasisi mbalimbali za Serikali wamefika mkoani Kigoma kwa lengo la usimamizi wa utekelezaji katika Mradi wa ujenzi wa Chuo cha TEHEMA  Wilaya ya Buhigwe.

Baadhi ya wajumbe wa Kamati inayoundwa na Wataalam kutoka taasisi za Serikali waliofika katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma wakifuatilia maelezo ya Mkuu wa Mkoa, Kamishna Mstaafu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Thobias Andengenye.

 ‘’Wawekezaji wengi wanashindwa kuungana nasi ili  kuwekeza katika Mkoa wa Kigoma kutokana na tatizo kukosekana kwa uUmeme wa kutosha wenye uhakika. Lakini tunaelekea kuzuri kwani Serikali yetu chini Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan, inaendelea kutekeleza Miradi mikubwa ya Umeme mkoani hapa’’ amesema Andengenye Mkuu wa Mkoa wa Kigoma.

Amesema hayo alipokutana na Timu ya Wataalam kutoka katika Taasisi mbalimbali za Serikali, iliyopo mkoani hapa kwa Lengo la usimamizi wa utekelezaji Mradi wa ujenzi wa Chuo cha TEHAMA katIka Wilaya ya Buhigwe.

Amesema kwa sasa Serikali inaendelea na ujenzi wa Mradi wa Umeme wenye Kilovoti 400 kutoka Nyakanazi hadi Kidahwe katika Wilaya ya Kigoma vijijini ambapo kukamilika kwa mradi huo kutamaliza kabisa adha ya Umeme mkoani hapa na kufungua fursa za uwekezaji hasa wa viwandani.

Dkt. Suleiman Daud kiongozi wa Timu ya Wataalam toka Taasisi za Serikali, amesema Kigoma ni Mkoa wa kimkakati hususani katika suala la Elimu kutokana na kupakana na Nchi za jirani, hivyo mahitaji ya umeme ni muhimu kwani  yanapaswa kwenda sambamba na maendeleo ya Teknolojia.

Amesisitiza kuwa, ujenzi wa chuo cha TEHAMA utafungua fursa kwa watanzania na Raia wa Kigeni kusoma katika chuo hicho, hivyo Miundombinu wezeshi ni muhimu katika kufikia malengo hayo.

‘’Tunaimani na Uongozi wa Mkoa pamoja na wilaya ya Buhigwe kwani viongozi waliopo ni mahiri na tunauhakika kuwa zoezi la Ujenzi wa chuo hicho litapata usimamizi wa kutosha na kukamilika kwa wakati’’ amesisitiza Dkt. Daud.

Chuo hicho kinatarajiwa kujengwa katika Kijiji cha Songambele wilayani Buhigwe Mkoani hapa, ambapo tayari wananchi wa Buhigwe wamekubali kutoa eneo la Ekari 149.9 kwa ajili ya ujenzi huo.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa