• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

KITUO CHA M-MAMA CHAZINDULIWA KIGOMA

Posted on: July 14th, 2023

Kituo cha kuratibu Mfumo wa Huduma ya Usafiri  wa Dharura kwa wajawazito, Mama na watoto wachanga (m-mama) umezinduliwa rasmi mkoani Kigoma na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Dkt. Jesca Lebba kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma.

Akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi huo iliyofanyika katika Hospitali ya Mkoa wa Kigoma Maweni, Dkt. Jesca Lebba amewataka  watendaji watakaohusika na uendeshaji wa mfumo huo kutanguliza uzalendo kwani ufanisi wake utachangia kwa kiasi kikubwa kupunguza vifo kwa wajawazito, wazazi na watoto.

Amesema mahitaji ya usafiri ni makubwa kwani magari hitajika kwa ajili ya kusafirisha wagonjwa kimkoa ni 50,  ambapo yaliyopo ni 24 huku upungufu ikiwa magari 26 sawa na asilimia 52.

Upande wake Mganga Mkuu Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa wa Kigoma Dkt. Stanley Binagi amesema ukosefu wa usafiri wa uhakika umekuwa ni changamoto iliyosababisha vifo vingi kwa makundi  hayo hivyo ujio wa mfumo huo utapunguza kwa kiasi kikubwa hatari ya vifo vya wanawake, wajawazito na watoto wachanga.

Ameendelea kusisitiza kuwa, kwa kushirikiana na wadau wa Huduma ya m-mama, watahakikisha Mfumo unafanya kazi wakati wote kutokana na Hospitali kupokea na kutoa huduma kwa wagonjwa wote wanaopewa rufaa kutoka Hospitali za wilaya mkoani Kigoma.

‘’Ili kutimiza malengo ya kuanzishwa mfumo wa m-mama, watendaji wanapaswa kushirikiana na kuhakikisha mfumo unakuwa wazi kiutendaji kwa Saa 24 kila siku ili uweze kutoa huduma nyakati zote’’amesema Dkt. Binagi.

Mfumo wa m-mama unaendeshwa na Serikali kwa kushirikiana na wadau ambao ni Vodacom, Touch Foundation pamoja na Pathfinder International.

Huduma ya m-mama mkoani Kigoma inapatikana kwa kupiga Namba ya Huduma 115 na wananchi wanashauriwa kutumia namba hiyo kwa dharura zinazohusu walengwa ili kuepusha hasara na matumizi yasiyo ya lazima kwa rasilimali za Serikali na upotevu wa muda kwa watendaji.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa