• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

KIPINDI CHA TAMISEMI KAZINI KUJA NA MAJIBU YA UTEKELEZAJI MIRADI YA SERIKALI

Posted on: August 14th, 2022

PICHA: BAADHI YA  MIRADI ILIYOTEMBELEWA NA TIMU YA  UTAYARISHAJI WA KIPINDI CHA TAMISEMI KAZINI MKOA WA KIGOMA.

Ujenzi wa Nyumba Tano  za watumishi wa Idara ya Afya katika Hospitali ya Wilaya ya Kasulu.  Ujenzi huo unaotekelezwa kutokana na Fedha za Mapato ya Ndani unna lengo la kupunguza adha kwa watumishi wa Hospitali hiyo kukaa mbali na Kituo cha kazi na kurahisisha upatikanaji wa huduma.

Ujenzi wa Jengo la kudhibiti Magonjwa ya Mlipuko (Isolation Centre) katika Kituo cha Afya Nyakitoto Wilayani Kasulu.       

Kitalu cha Miche ya zao la Chikichi kilichopo katika Manispaa ya Kigoma-Ujiji.

Kituo cha Afya Buhanda Manispaa ya Kigoma Ujiji.

Katika kuhakikisha Umma unahabarika na kupata taarifa mbalimbali za kazi zinazofanywa na Serikali,  Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa kushirikiana na Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) imeanzisha Kipindi Maalum cha Televisheni Kiitwacho TAMISEMI KAZINI.

Bi Angela Msimbira Afisa Habari Mkuu TAMISEMI anayeongoza Timu ya utayarishaji wa  kipindi hicho, amesema walengwa wa kipindi ni Wananchi ambao wanataka kufahamu matumizi ya kodi zao kupitia shughuli mbalimbali zinazoendelea kutekelezwa na Serikali kwa lengo la kuwaletea Maendeleo.

Afisa habari huyo amesema wameridhishwa na ushirikiano waliopewa  na Wakurugenzi pamoja na  wakuu wa Idara katika zoezi la kutembelea miradi iliyopendekezwa kutembelewa  kwa ajili ya upigaji picha pia ushiriki mzuri katika utoaji wa taarifa kupitia mahojiano yaliyofanyika  kwa  lengo la uandaaji wa kipindi.

Upande wake Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye ameipongeza Wizara ya Ofisi ya Rais- TAMISEMI  kwa kuanzisha kipindi hicho Maalum cha Runinga ambacho kitawafanya wananchi kufahamu kazi zinazofanywa na Serikali na kupunguza sintofahamu kuhusu utekelezaji wa miradi mbalimbali.

Mkuu huyo wa Mkoa ametoa pongezi hizo mara baada ya kumaliza sehemu yake katika maandalizi ya  kipindi hicho ambapo ameshirki katika mahojiano yaliyofanywa na Nguli wa uandaaji wa vipindi na utangazaji, Asheri Thomas kutoka Shirkia la Utangazaji la Taifa.

‘‘Nimefurahishwa na uanzishwaji wa kipindi hiki, kwani kitasaidia kuwafahamisha wananchi kuhusu kazi mbalimbali zinazofanywa na Serikali zikiwa na lengo la kuboresha maisha yao na kuwafanya waishi katika kiwango bora’’ amesema Andengenye.

Zoezi hilo limefanyka katika Manispaa ya Mji  Kigoma-Ujiji, kisha kuendelea katika Wilaya za Kasulu na Uvinza ambapo miradi mbalimbali imetembelewa kupigwa picha na kufanyika kwa mahojiano.

Aidha kipindi hicho kimelenga kuangazia taarifa za ukusanyaji wa mapato ya ndani , utoaji wa mikopo ya Asilimia Kumi na Miradi inayotekelezwa kwa fedha zitokanazo na mapato ya ndani.

Mkoa wa Kigoma umechaguliwa kuwa wa kwanza katika uandaaji wa Kipindi cha TAMISEMI KAZINI kinachotarajiwa kuanza kurushwa hewani na kituo cha Runinga cha Taifa (TBC ONE).

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa