• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

KIGOMA YAWEKA MIKAKATI KUIMARISHA UKUSANYAJI WA MAPATO YA NDANI

Posted on: July 17th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye amewataka watendaji katika Taasisi za Umma na Halmashauri mkoani hapa kuongeza ubunifu katika kubaini vyanzo vya mapato ili kuongeza kuinua kiwango cha makusanyo katika Halmashauri na kuziwezesha kumudu kujiendasha sambamba na kutekeleza miradi mbalimbali ya Maendeleo.

Mhe. Andengenye ametoa kauli hiyo alipozungumza kwenye Kikao kilichowakutanisha  wataalam kutoka Taaasisi za Umma pamoja na watendaji kutoka mamalaka za serikali za mitaa  mkoani hapa kikilenga kujadili na kubaini fursa mbalimbali za kiuchumi zilizopo kwenye mkoa wa Kigoma na kupanga mikakati ya namna bora ya kuzitumia ili kuimarisha ukusanyaji wa mapato.

Amesema mko una vyanzo vingi vya Mapato, kinachotakiwa ni ubunifu katika ubainifu  wa vyanzo hivyo ili viweze kuleta tija katika uzalishaji na ukusanyaji wa mapato, jambo litakaloimarisha uchumi wa mkoa na nchi kwa ujumla.

Aidha Mkuu huyo wa Mkoa amewataka watendaji hao kujenga utamaduni wa kutoa huduma bora kwa wananchi jambo litakalowezesha wapokea huduma kuzitangaza kazi nzuri zinazofanywa na serikali mkoani hapa.

Awali akizungumza kabla ya kumkaribisha Mkuu huyo wa Mkoa, Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma Hassan Rugwa amesema lengo la kikao hicho ni kufanya mapitio ya vyanzo vya mapato vya taasisi za Umma mkoani hapa na kuona namna bora ya kuongeza makusanyo ya ndani.

Amesema malengo ya mkoa ni kuhakikisha kwa kipindi cha Mwaka wa Fedha 2024/2025 malengo ya makusanyo kimkoa hadi ifikapo 20230 ni kufikia kati ya shilingi Bil.20 hadi 25.

Aidha Rugwa amewataka watendaji hao kwenda kuibua vyanzo vipya vya mapato katika maeneo yao wanayoyasimia na kuondoa vyanzo visivyo na tija.

‘’Hakikisheni mnaandaa mazingira bora ya ukusanyaji wa mapato, kuondoa tozo zinazoweza kuwaletea kero wananchi sambamba na kuandaa mazingira yatakayotoa fursa kwa wawekezaji ili waweze kuwekeza katika maeneo yenye vivutio vya uwekezaji’’ amesema Rugwa.

Upande wake Mkuu wa Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mkoa Ndg. Deogratius Sangu amesema  kikao hicho cha wataalam wa mkoa kimehusisha wakuu wa Taasisi za Umma zilizopo mkoani humo, Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa, wachumi, wataalam wa mipango na mipango miji pamoja na Maafisa biashara lengo kuu likiwa kuhakikisha  wataalam hao wanajengewa uwezo katika kubaini na kuhakikisha wanatumia vursa za kiuchumi zilizopo mkoani humo kwa ajili ya kuleta maendeleo ya wananchi.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa