• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

KIGOMA YANG'ARA TUZO NBAA

Posted on: December 10th, 2024

Watendaji wa Serikali mkoani Kigoma wametakiwa  kuzingatia Miongozo ya matumizi ya Fedha za Umma ili kufanikisha mipango ya Serikali inayolenga kuimarisha utoaji huduma kwa wananchi.

Wito huo umetolewa na Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma Hassan Rugwa alipozungumza katika hafla fupi ya kimkoa mara baada ya kukabidhiwa  tuzo ya umahiri katika Uandaaji wa Hesabu za Fedha kwa kuzingatia viwango vya kimataifa vya uhasibu Sekta ya Umma kwa mwaka 2022/2023 iliyotolewa na bodi ya Taifa ya wahasibu na wakaguzi Tanzania (NBAA) ambapo mkoa umeshika nafasi ya tatu kipengele cha mikoa.

Amesema katika namna ya pekee anatoa pongezi kwa watendaji wote kwa ushirikiano wao uliosababisha mkoa wa Kigoma kuendela kushika nafasi za juu kwa kipindi cha miaka sita.

"Kwetu tuzo hii inatoa tafsiri pana na kuonesha kuwa tunatekeleza majukumu kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na Taratibu za Matumizi ya Fedha kuanzia upangaji wa bajeti na mlolongo wa utekelezaji wa bajeti hiyo katika mkoa na mamlaka za Serikali za Mitaa" amesisitiza Rugwa.

Aidha amemshukuru Rais  Dkt. Samia kwa kuendelea kuufungua mkoa ikiwemo kuimarisha miundombinu ya kutolea huduma za jamii jambo litakalotoa fursa kwa wananchi kupata huduma bora sambamba na kuzidi kufungua fursa za  kiuchumi.

Johson Gamba, Muhasibu Mkuu wa Mkoa amesema mkoa umeendelea kupata tuzo hiyo kwa miaka sita ikiwa ni ishara ya uongozi wa mkoa wa Kigoma kusimamia vizuri fedha zinazotolewa na serikali katika kutekeleza kazi na miradi mbalimbali ya Maendeleo.

"Ni vizuri watendaji wote tunaohusika na matumizi ya fedha  ngazi ya mkoa na halmashauri  kuhakikisha tunaendelea kuimarisha na kuzingatia mifumo ya ndani ya usimamizi na matumzi ya fedha  za Umma" amesema Gamba.

Amesema ni muhimu kwa wakuu wa Idara, vitengo na sehemu kuhakikisha watendaji walio chini yao wanafahamu michakato yote ya matumizi ya  fedha katika eneo lao sambamba na kujengewa uwezo wa kuzingatia kanuni na miongozo ya matumizi ya fedha za Umma.


Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa