• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

KIGOMA YAJIPANGA KUONGEZA UFANISI KATIKA KUFANIKISHA AFUA ZA LISHE

Posted on: October 26th, 2022

Serikali Mkoani Kigoma imejipanga kuongeza ufanisi katika kuinua kiwango cha utekelezaji wa Afua za Lishe kufuatia Mkoa kushika nafasi ya 22 kitaifa kati ya Mikoa 26 ya Tanzania Bara kwa mujibu wa takwimu zilizotokana na Tathmini ya Afua za Lishe Kitaifa kwa kipindi cha Mwaka 2021/2022. 

Mkakati huo wa Pamoja umewekwa kwenye Kikao cha kusaini Mkataba Tendaji wa Lishe ngazi ya Jamii baina ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Wakuu wa Wilaya, pamoja na wakurugenzi wa Halmashauri mkoani  hapa, kikiwa na lengo la kufanikisha suala la kuboresha hali ya lishe na kupunguza athari za utapiamlo katika jamii pamoja na kufuatilia maendeleo ya utekelezaji wa mpango huo kwa ngazi ya Halmashauri.

Akifungua kikao hicho kilichofanyika katika Halashauri ya Mji wa Kasulu, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye alisema, kigezo kilichosababisha mkoa kushika nafasi hiyo ni kiashiria cha utoaji Fedha ambapo kwa kipindi cha Mwaka 2021/2022 kilitolewa kiasi cha Shilingi 630 badala ya Shilingi 1000 kwa kila mtoto mwenye umri wa chini ya Miaka mitano na kusababisha Mkoa kutoa Asilimia 80 ya Fedha ya Afua za Lishe.

‘’Kila halmashauri inajukumu la kutenga kiasi cha Shilingi 1000 kwa kila mtoto chini ya miaka mitano kwa lengo la kupunguza udumavu na kuimarisha afya zao kupitia upatikanaji wa lishe bora katika maeneo ya mkoa wetu, aidha kutokufanya hivyo ni kuwanyima watoto hao haki yao ya kimakuzi’’ alisema.

Alisistiza kuwa, halmashauri zote zihakikishe  Fedha iliyotengwa kwa ajili ya Afua za Lishe kwa kipindi cha 2022/2023 inalingana na idadi ya watoto walio chini ya  umri wa miaka mitano na iwapo bajeti iliyopangwa ni pungufu, marekebisho yafanyike haraka ili changamoto hiyo isijirudie.

‘‘Halashauri zihakikishe fedha iliyotengwa inatolewa yote na isitumike kwa kutekeleza shughuli nyingine tofauti na Afua za Lishe’’ alisema Andengenye.

Naye Mkuu wa wilaya ya Kibondo Kanali Agrey Magwaza, alisema kwa kushirkiana na wakurugenzi wa Halashauri, wamekubaliana  kuhakikisha kila robo itolewe Shilingi 250 ili ifikapo mwisho wa Mwaka ipatikane Shilingi 1000 kwa lengo la  kufikia kigezo cha Utoaji fedha kama kilivyowekwa na Serikali.

Aidha, amewataka maafisa Lishe wawe wanatoa taarifa ya maendeleo ya ukusanyaji na uwasilishaji wa Fedha hiyo kwa wakuu wa wilaya ili kuwarahisishia ufuatiliaji wa fedha hiyo ili kubaini changamoto zinazoweza kujitokeza na kushauri namna ya kuzitatua.

Awali akitoa taarifa ya utekelezaji wa viashiria na utatuzi wa Afua za Lishe, Afisa Lishe Mkoa wa Kigoma  Naomi Lumenyela, alisema wakurugenzi wanapaswa kutoa fedha kuendana na Muongozo wa Serikali huku akisisitiza wazazi kuzingatia miongozo ya ulishaji wa chakula kwa watoto pamoja na utoaji wa Elimu ya Lishe kwa Jamii ili kupunguza tatizo la utapiamlo na udumavu.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa